Mkurugenzi wa Elimu ya Juu Toka Wizara
ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi Prof.
Sylvia Temu akiwaeleza waandishi wa habari leo Jijini Dar es salaam hawapo (pichani)
kuhusu umuhimu wa jamii kuchangia katika sekta ya elimu ya Juu ili kupanua
zaidi wigo wa wanafunzi wanaojiunga na Elimu
hiyo. (Picha zote na Frank Mvungi-Maelezo)
Na Frank
Mvungi-Maelezo
WAKALA wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) Wahimiza wananchi kote nchini kushiriki
katika ufugaji wa nyuki ili kuongeza
vipato vyao na kuchangia katika kukuza uchumi wa Taifa.
Hayo
yamesemwa na Ofisa Ufugaji Nyuki
Mwandamizi wa wakala huo Bw. Steven Msemo jana, jijini Dar es Salaam wakati wa
mkutano na waandishi wa habari uliolenga kuhamasisha jamii kushiriki katika
ufaugaji wa nyuki.
Akifafanua
Msemo amebainisha kuwa mizinga ya nyuki takribani 14,000 imetengenezwa na kugawiwa wananchi
wanaoishi jirani na Misitu ikiwa ni moja ya mikakati ya Serikali katika kukuza
sekta hiyo.
“Wakala
wa Huduma za misitu Tanzania kama Taasisi inayo mizinga 3,870 iliyo katika
manzuki mbalimbali katika kanda saba na katika mashamba ya miti kwa lengo la
kuzalisha na sehemu ya mafunzo kwa jamii “alisisitiza Msemo
Katika
kuwajengea uwezo wananchi Msemo amebainisha kuwa Wataalamu wa ufugaji nyuki
wamekuwa wakiwajengea uwezo wananchi kwa kuwapa mbinu za kusimamia makundi ya
nyuki na kuzalisha malkia ili kuondokana na mazoea ya kutundika mizinga na
kuacha hadi kipindi cha mavuno.
Aidha,
Wakala umekuwa ukihamasisha asasi
zinazojikita na kutengeneza vifaa vya ufugaji nyuki kuzingatia utaalamu na
vipimo vya mizinga.
Tanzania
ni moja kati ya nchi zenye utajiri mkubwa wa makundi ya nyuki yenye uwezo wa
kuzalisha asali na mazao mengine ya nyuki mfano Nta,Gundi ya nyuki na chavua.
No comments:
Post a Comment