TANGAZO


Wednesday, October 30, 2013

Majaji kutoa uamuzi wa hukumu ya Babu Seya

Nsanii wa muziki wa dansi, Nguza Vicking 'Babu Seya' akiwa na Mwanawe Johnson Nguza 'Papii kocha', katika chumba cha Mahakama ya Rufaa Tanzania jijini Dar es Salaam leo, kabla ya kuanza kwa kusikilizwa kwa rufaa yao ya kuitaka mahakama hiyo kupitia upya hukumu iliyotolewa Februari 10-2010 na mahakama hiyo. Nguza na Papii walihukumiwa kifungo cha maisha jela baada ya kupatikana na hatia ya ubakaji na ulawiti. (Picha zote kwa hisani ya Francis Dande)
Watu waliohudhuria mahakamani hapo wakifuatilia kesi hiyo.
Nguza Vicking 'Babu Seya' akiwa na Mwanawe Johnson  Nguza au Papii wakiwa katika chumba cha Mahakama ya Rufaa Tanzania kabla ya kuanza kwa kusikilizwa kwa rufaa yao, ya kuitaka Mahakama hiyo kupitia upya hukumu iliyotolewa Februari 10-2010 na mahakama hiyo.  

Wakiwa mahakamani leo.

Nguza Vicking 'Babu Seya' akiwa na Mwanawe Johnson  Nguza wakiteta jambo na wakili wao, Mabere Marando.
Nguza Vicking 'Babu Seya' akiwa na Mwanawe Johnson  Nguza 'Papii' wakiwa na nyuso za furaha wakati wakitoka katika Mahakama ya Rufaa baada ya majaji wa Mahakama ya Rufaa Tanzania kusikiliza maombi yao ya kuitaka mahakama hiyo, kupitia hukumu iliyoitoa mwaka 2010.
Nyuso za matumaini.......

Johnson  Nguza 'Papii' akibusu mkono wake baada ya kuibusu ardhi mara baada ya kutoka mahakamani hapo.
Papii akinyoosha mkono juu kama ishara ya kumshukuru mungu.
Waandishi wa habari wakiwa chini wakati wa harakani za kuchukua matukio mahakamani hapo.


Nguza Vicking 'Babu Seya' akiwa na Mwanawe Johnson  Nguza wakati wakitoka mahakamani.

No comments:

Post a Comment