TANGAZO


Wednesday, September 4, 2013

Tumieni Nishati mbadala katika Maendeleo - Mulongo

Catherine Peter, mkazi wa Sombetini - Arusha, akitoa maelezo kwa Ofisa Tawala wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Arusha, Lemueli Kileo, namna kifaa cha umeme jua kinavyofanya kazi baada ya kuwa Mtanzania wa 1000 kuunganishwa na nishati hiyo na Kampuni ya Mobisol, umeme huo unaunganishwa kwa wakazi wa maeneo ya vijijini kwa mkopo na kulipa kupitia Vodacom M – PESA. Wanaoshudia kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Mobisol, Allan De Mello na Meneja wa Vodacom Mkoa wa Arusha, Philemon Chacha.

Catherine Peter, mkazi wa Sombetini - Arusha, akitoa maelezo kwa Ofisa Tawala wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Arusha, Lemueli Kileo, namna kifaa cha umeme jua kinavyofanya kazi baada ya kuwa Mtanzania wa 1000 kuunganishwa na nishati hiyo na Kampuni ya Mobisol, umeme huo unaunganishwa kwa wakazi wa maeneo ya vijijini kwa mkopo na kulipa kupitia Vodacom M – PESA. Wanaoshudia kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Mobisol, Allan De Mello na Meneja wa Vodacom Mkoa wa Arusha, Philemon Chacha.

Ofisa Tawala Ofisi ya Mkuu wa Wilaya Arusha, Lemueli Kileo, akiwasha mtambo wa 1000 wa Umeme Jua Nyumbani kwa Catherine Peter ambaye ni Mtanzania wa 1000, kuunganishwa na matumizi ya umeme jua na Kampuni ya Mobisol, umeme huo unaunganishwa kwa wakazi wa maeneo ya vijijini kwa mkopo na kulipa kupitia Vodacom M – PESA. Wanaoshihudia kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Mobisol, Allan De Mello na Meneja wa Vodacom Mkoa wa Arusha, Philemon Chacha.

Baadhi ya waandishi wakiwa katika hafla hiyo.


MKUU wa mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo ametoa wito kwa jamii ya watanzania kujenga utamaduni wa kutumia njia mbadala za kuzalisha nishati badala ya kuendelea kutegemea serikali kusambaza umeme kutoka katika gridi ya taifa.
Hayo yamesemwa na Afisa Tawala Ofisi ya Mkuu wa Wilaya Arusha, Bwana, Lemueli Kileo  wakati akisoma hotuba ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha katika hafla ya kumkaribisha mteja wa 1,000, aliyefungiwa Mtambo wa sola wa nyumbani na kampuni ya Mobisol  Mkoani Arusha.
Mkuu huyo wa mkoa amesema Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali kupitia wakala wa Umeme vijijini REA wameweka malengo kuhakikisha sehemu zote zilizo nje ya gridi ya taifa zinapata nishati ya umeme.
“Ninawapongeza Vodacom wakishirikiana na Mobisol kutoka Ujerumani  ambao ni wasambazaji wa nishati ya umeme jua kwa njia ya teknolojia ya simu za mkononi, kwa kuwawezesha Watanzania hasa wa maeneo ya vijijini wanapata nishati hiyo.” Alisema na kuongeza.
“Ninatoa wito kwa Watanzania kutumia fursa hii ya kipekee katika kupata nishati kuliko kutegemea serikali ifikishe Umeme katika maeneo yao kutoka katika gridi ya taifa, hili litawawezesha watanzania zaidi kupata nishati kiurahisi zaidi.
Kwa upande wake Afisa Mahusiano wa REA Bi. Jaina Msuya amesema kuwa wakala huyo amefurahia ushirikiano huo ambao umewezesha watanzania zaidi kupata nishati ya umeme, Hivyo wao kama wakala wako tayari kushirikiana na wadau mbalimbali kwa kutoa Ruzuku ambazo zitawawezesha wadau mbalimbali kufikisha umeme vijijini.
“Sisi ni moja ya Taasisi za serikali zinazotekeleza mpango wa serikali wa matokeo makubwa “Big Result” hivyo mafanikio haya ni moja ya mafanikio ya utekelezaji wa mpango huo.”
Bibi Catherine Peter, ambaye ni mteja wa mteja wa 1,000  wa Mobisol amesema ‘’ Mimi nafurahia sana kuweza kumiliki mtambo wangu wa kwanza ambao unaotumia nishati ya umeme jua, yaani Solar Home System, Nashukuru sana mfumo wa kulipia kiasi kidogo kidogo cha pesa kwa mwezi, unaoniwezesha kumudu kabisa kujipatia mtambo mkubwa wa watts 120, Alisema na kuongeza,
“Natumia mtambo huu wa solar kuangaza nyumba yangu. Watoto wangu sasa na wajukuu wanaweza kujisomea usiku bila matatizo ya mwanga na pia nina mpango wa kuanzaisha biashara ya kuchaji simu za majirani zangu”
Mtambo wa 1,000 uliwashwa rasmi na Bwana Lemueli Kileo Kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa Magesa S. Mulongo. Baada ya mazungumzo na wanahabari waliokuwepo kwenye sherehe pamoja na vingozi waalikwa kutoka serikalini.
Bwana Thomas Gottschalk, Meneja Mkuu wa kampuni ya Mobisol amesema: “Tumefanikiwa kubuni mtambo wa bei nafuu ambao wengi wanaweza kumudu bei yake, ina kidhi mahitaji ya kisasa ya kiteknologia yenye ubora na ya kudumu. 
Kwa mfumo wa kufua nguvu za nishati ya umeme wa jua au kwa lugha rahisi kuvuna nguvu za Jua.
Mobisol imeweza kutunza mazingira husika na kuinua hali ya uchumi ya wateja wake sambamba na kuwangaza majumbani.
“Leo tunasherekea ufungaji wa mtambo wa 1,000 Tanzania, kesho tunatarajia kwa kiasi kikubwa kuwa uvumbuzi wa sola itainua na kubandilisha maisha ya mamilioni barani Afrika” alisema Bwana Gottschalk.
Kwa upande wake, Mkurugenzi mtendaji wa Vodacom Rene Meza, amesema Vodacom kupitia M pesa wameendelea kurahisisha maisha ya mamilioni ya Watanzania.
“M–pesa inaendelea kuwa pendekezo la ufumbuzi wa malipo kwa Watanzania leo na sisi tuliopo Vodacom tutaendelea kujizatiti kuwapatia wateja wetu bidhaa na huduma bora zinazoendana na mwenendo wa maisha yao.” Rene Meza
 “M-pesa leo imekuwa muundo mbinu ya lazima, yaani imefanya mapinduzi ya maisha kwa mamilioni ya Watanzania ambao huitegemea kwa huduma za kifedha ambazo tofauti  zinatolewa na mawakala wetu 50,000 wa M-pesa kote nchini.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Kusambaza Teknolojia ( KAKUTE LTD)  kutoka Arusha, Ndugu Livinus S. Manyanga pia aliainisha kwamba KAKUTE ilikuwa funguo kwa kutoa ushirikiano wa awali wa Wafanyakazi na maendeleo ya soko la awali ambalo Mobisol walihitaji kwa ukuaji wa biashara yake ndani ya Arusha tangu ulipoanza mradi wa awali wa majaribio. Aliongeza kwamba KAKUTE ilichangia kujenga msingi wa upanuzi wa biashara tangu mwanzo kwa uaminifu uliojijengea na serikali pamoja na taasisi za kusambaza nishati kote Tanzania.

No comments:

Post a Comment