TANGAZO


Friday, December 8, 2017

RAIS DKT. SHEIN AWASILI MKOANI DODOMA KUHUDHURIA SHEREHE ZA UHURU WA TANZANIA BARA KESHO

 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Dodoma na kusalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Kondoa Mhe Sezaria Makota, kwa ajili ya kuhudhuria Sherehe za Miaka 56 ya Uhuru wa Tanzania Bara zitakazofanyika katika uwanja wa Jamuhuri leo.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akisalimiana na Katibu Mkuu wa UVCCM, Shaka Hamdu Shaka alipowasili Uwanja wa Ndege wa Dodoma kuhudhuria sherehe za Uhuru wa Tanzania Bara zinazofanyika katika Uwanja wa Jamuhuri.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein, akisalimiana na Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama Mkoani Dodoma alipowasili katika uwanja wa ndege kwa ajili ya kuhudhuria sherehe za Uhuru wa Tanzania Bara kesho katika viwanja vya Jamuhuri Dodoma.(Picha zote na Othman Maulid)  

No comments:

Post a Comment