TANGAZO


Friday, December 8, 2017

UZALENDO NA UTAIFA KAMPENI KUZINDULIWA LEO NA RAIS JOHN POMBE MAGUFULI



LEO ni siku ya Uzinduzi wa kampeni ya Uzalendo na Utaifa. Uzinduzi huo utafanyika katika ukumbi wa Chimwaga Dodoma,  kwa ratiba itakayoanza saa 9 mchana na kuisha saa 3 usiku.. Kati ya matukio yatakayokuweko ni maandamano yatakayoshirikisha wasanii mbalimbali na pia kazi za sanaa, baada ya watu wote kufika na kutulia Chimwaga kutakuweko na wimbo maalumu wa Uzalendo, filamu ya kihistoria, hotuba za viongozi wastaafu, uzinduzi wa kitabu, na kisha Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania atatoa vyeti vya udhamini hatimae chakula. Wimbo hapo juu ni kazi ya wanamuziki Anania Ngoliga na John Kitime wakipiga gitaa na rimba kuisifia nchi yao,

No comments:

Post a Comment