TANGAZO


Wednesday, November 22, 2017

Mladic apewa kifungo cha maisha kwa mauaji ya kimbari Bosnia

Jenerali Ratko Mladich

Image captionJenerali Ratko Mladich
Kamanda wa zamani wa jeshi la Boznia Jenerali Ratko Mladich amehukumiwa maisha jela na Mahakama ya kimataifa ya makosa ya uhalifu wa kivita-ICC.
Mladich alipatikana na hatia ya kutekeleza mauaji ya kimbari na uhalifu wa kivita pamoja na dhulma dhidi ya binadamu katika iliyokuwa utawala wa Yugoslavia.
Hukumu imepokelewa kwa hisia tofauti.
Kundi la wamama wa Srebrenitsa, limesema kuwa limefurahishwa mno na hukumu hiyo.
Lakini mwanamke mmoja Muislamu raia wa Boznia, ambaye wavulana wake wawili na mumewe waliuwawa katika vita hivyo, ameiambia bbc kuwa Bwana Mladich anastahili hukumu kubwa na kali zaidi.
Mwaandishi wa BBC huko Sarayevo, anasema kuwa watu wengi walitaka ahukumiwe kwa mauwaji yote yaliyotokea kote Boznia na wala sio eneo moja pekee.

No comments:

Post a Comment