TANGAZO


Friday, October 7, 2016

ZIARA YA JAJI MKUU WA AUSTRALIA KATIKA MAHAKAMA YA KISUTU JIJINI DAR ES SALAAM LEO

Jaji Mkuu wa  Australia  ya Kusini, Mhe. Christopher Kourakis (kushoto), akipokea zawadi ya picha kutoka kwa  Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Mohamed Chande Othman (kulia) katika halfla fupi iliyofanyika leo tarehe 7.10 .2016 kwenye ukumbi wa maktaba wa  Mahakama  ya Rufani  ya Tanzania. 
Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (kushoto), akizungumza  na Jaji Mkuu wa  Australia  ya Kusini, Mhe. Christopher Kourakis(katikati) na (kulia) ni Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania,Bi.  Katarina  Revocati katika mkutano  huo ulifanyika leo tarehe 7.10 .2016 kwenye ukumbi wa mikutano wa Wizara ya Katiba  na Sheria uliopo jijini Dar es Salaam. 
 Jaji Mkuu wa  Australia  ya Kusini, Mhe. Christopher Kourakis (kulia) akizungumza kuhusu ziara yake ya siku tatu aliyoifanya nchini na kubadilishana uzoefu wa masuala mbalimbali ya mafunzo, sheria na shughuli za kimahakama baina ya nchi hizo mbili. (Kushoto) ni Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe. Mkutano  huo ulifanyika leo tarehe  7.10.2016 kwenye ukumbi wa mikutano wa Wizara ya Katiba  na Sheria uliopo jijini Dar es Salaam.
Jaji Mkuu wa Australia ya Kusini, Mhe. Christopher Kourakis akiangalia na kupata  maelezo juu  ya mfumo wa kielektroniki wa kusajili  mashauri kutoka kwa Karani wa Mahakama ya Hakimu Mkazi  Kisutu, iliyopo jijini Dar es Salaam Bw. Abdalla Bugalo wakati alipoitembelea leo tarehe 7.10 .2016. (Picha zote na Mahakama ya Tanzania)

No comments:

Post a Comment