Waziri wa Afya, maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiongea na Mkuu wa Mkoa wa Kagera na kuipongeza kamati ya mkoa kwa namna walivyojipanga kukabiliana na athari za tetemeko pamoja na kuwahudumia waathirika.
Waziri wa Afya, maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akimkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum Kijuu misaada iliyotolewa na Bohari ya Madawa (MSD) waliotoa Dawa na Vifaa tiba vyenye thamani ya shilingi milioni 30.
Waziri
wa Afya, maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akimkabidhi
Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum Kijuu mashuka 250
yaliyotolewa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF).
Na
Eleuteri Mangi-Maelezo
WAZIRI wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu ameahidi
kutuma timu ya wataalam kutoka Idara ya Magonjwa ya Mlipuko ili kuja
kushirikiana na timu ya Mkoa ili kufanya tathmini ili kuweza kuepusha magonjwa
ya mlipuko hasa katika kipindi hichi ambacho mvua zimeanza kunyesha mkoani
humo.
Akiongea
wakati akikabidhi misaada kwa mkoa wa kagera Meja jenerali Mstaafu Salum Kijuu
Waziri Ummy amesema anatambua kipindi hiki cha mvua huwa ni tishio kwa magonjwa
ya mlipuko hivyo wizara itachukua hatua ya kutuma wataalam pamoja na kutoa
elimu ya jinsi ya kujikinga na magonjwa hayo.
“Nafahamu
tuko kwenye kipindi cha mvua nyingi ambacho mara nyingi magonjwa ya mlipuko
ikiwemo kipindupindu huibuka, hivyo kabla ya hayo kutokea kama tahadhari sisi
kama wizara tutatuma wataalam kuja kufanya tathmini na kutoa elimu ya namna ya
kujikinga” Alisema Waziri Ummy.
Aidha
Waziri Ummy amekabidhi misaada ya Dawa na Vifaa vyenye thamani ya shilingi
milioni 30 vilivyotolewa na Bohari kuu ya Dawa (MSD) kwa mkuu wa mkoa wa kagera
Meja jenerali Mstaafu Salum Kijuu kwa ajili ya kusaidia waathirika wa tetemeko
mkoani humo.
Pia
Waziri Ummy amekabidhi mashuka 250 yaliyotolewa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya
Afya (NHIF) kwa ajili ya Hospitali, Vituo vya Afya na Zahanati mkoani kagera.
Akiwa
katika ziara kutembelea maeneo yaliyoathiriwa na tetemeko la ardhi Waziri Ummy
amewataka watumishi katika sekta ya afya mkoani humo kuweka mkakati wa kuweka
mazingira safi kwenye maeneo yote yaliyoathiriwa na tetemeko.
Wakati huo huo Waziri
Ummy ametembelea Kituo cha kulea wazee na watu wasiojiweza cha Kiilima
kilichopo katika Halmashauri ya Bukoba na kuagiza wazee hao kupatiwa chakula
cha milo mitatu ili kulinda afya zao.
Akizungumza
baada ya kupokea misaada hiyo mkuu wa mkoa wa kagera Meja jenerali Mstaafu
Salum Kijuu amewaomba wadau wengine kuendelea kutoa misaada kwa ajili ya
kurejesha hali baada ya maafa kutokea.
No comments:
Post a Comment