Baadhi ya Waandishi wa habari wakifuatilia mkutano wa
Mamlaka ya Udhibiti Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra) na vyombo
vya habari uliofanyika leo jijini Dar es salaam ukilenga kuhamasisha wadau wa
Sekta hiyo kuzingatia Sheria na Kanuni zinazosimamia Sekta hiyo.
Frank Mvungi-Maelezo
MAMLAKA ya
Udhibiti Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA) kwa kushirikiana na Jeshi la
Polisi,Kikosi cha Usalama Barabarani wamefanya ukaguzi katika Jiji la Dar es Salaam, ambapo wamefanikiwa kukamata mabasi
105 na kati hayo 36 yamefikishwa mahakamani baada ya
kukiuka wa masharti ya leseni ya usafirishaji abiria.
Akifafanua
Mziray amesema kati ya Machi 21-24 , 2016 ilifanya ukaguzi huo na ili sheria iweze kuchukua mkondo wake Kwa
wale wanaokwenda kinyume na taratibu zilizowekwa.
“Katika
kuimarisha huduma za usafiri Mamlaka imeweka utaratibu maalum wa kufanya ukaguzi
katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es salaam ikiwemo katikati ya
jiji,Ubungo,Buguruni na Kariakoo ili kubaini wale wote wanaovunja sheria”.alisisistiza
Mziray.
Akizungumzia
baadhi ya makosa yalibainika kutendwa na mabasi hayo Mziray alisema kuwa ni
pamoja na kuongeza nauli,kukata njia,kutoa huduma bila leseni ya
usafirishaji,kutoa huduma katika njia ambazo hawakupangiwa.
No comments:
Post a Comment