TANGAZO


Saturday, August 22, 2015

Mafunzo ya huduma za leseni kwa njia ya Mtandao mkoani katavi - 22/08/2015

Mwenyekiti wa Chama cha Wachimbaji Wadogo wa Madini mkoa wa Katavi (KATAREMA), William Mbogo (kushoto) akifuatilia mafunzo husika. Kulia ni Mhandisi Gilliard Luyoka. (Picha zote na Mohamed Seif-Wizara ya Nishati na Madini.
Mhandisi Gilliard Luyoka akizungumza kwa niaba ya Kamishna Msaidizi wa Madini Kanda Magharibi-Mpanda wakati wa mafunzo hayo.
Baadhi ya wachimbaji wadogo wa madini wakifuatilia mafunzo hayo. 
Mwenyekiti wa KATAREMA, William Mbogo (kulia) akiuliza swali kwa Mtaalamu kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Idd Mganga (kushoto), akimsiliza kwa ajili ya kumpatia jibu. 
Baadhi ya wachimbaji wadogo wa madini wakifuatilia mafunzo hayo. 
Mtaalamu kutoka Wizara ya Nishati na Madini Kitengo cha Leseni, Idd Mganga akiwasilisha mada wakati wa mafunzo hayo.

Na Mohamed Seif, Nishati na Madini
HATIMAYE mafunzo ya matumizi ya mfumo wa huduma ya leseni kwa njia ya mtandao yaani Online Mining Cadastre Transactional Portal (OMCTP) kwa wachimbaji madini mkoani Katavi yamemalizika. 

Mafunzo hayo ya siku moja yamefanyikia kwenye ukumbi wa mikutano wa Idara ya Maji, mjini Mpanda na kuhudhuriwa na wachimbaji wadogo wa madini kutoka maeneo mbalimbali ya mkoa huo yakiwa yamelenga kuwapatia uwezo wachimbaji madini wa kuutumia mfumo huo.

Akizungumza kwa niaba ya Kamishna Msaidizi wa Madini Kanda Magharibi-Mpanda, Mhandisi Gilliard Luyoka aliwakumbusha wachimbaji hao kuhakikisha wanafika kwenye Ofisi ya madini ili kusajiliwa kwa ajili ya kutumia mfumo huo.

Pamoja na malengo mengine, inaelezwa kwamba Mfumo huo umeanzishwa ili kutekeleza agizo la Serikali la kutaka Wizara na taasisi za Serikali ziwe zinapokea malipo ya Serikali kwa njia za kielektroniki.


Mfumo wa Huduma za Leseni kwa njia ya mtandao ulizinduliwa rasmi mnamo tarehe 8 Juni, 2015. 

No comments:

Post a Comment