Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein akisalimiana na Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Ulinzi wa Tanzania Luteni Jenerali Samuel Albert Ndomba wakati alipofika katika Kambi ya Ali Khamis Vitongoji Wilaya ya Chake Cahke Pemba leo akiwa katika ziara maalum kuzindua miradi mbali mbali ya Maendeleo ikiwa ni katika shamra shamra za miaka 51 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar. (Picha zote na Ikulu)
Baadhi ya wananchi waliohudhuria katika sherehe za uwekaji wa Jiwe la Msingi Ujenzi wa Nyumba za Makaazi ya Wanajeshi wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania ka(JWTZ) katika Kambi ya Ali Khamis Vitongoji Wilaya ya Chake chake Pemba leo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein akitoa hutuba yake wakati wa uwekaji wa jiwe la msingi ujenzi wa Nyumba za Makaazi ya Wanajeshi wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Vitongoji Wilaya ya Chake chake Pemba leo,ikiwa katika sherehe za shamra shamra za miaka 51 ya mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein akifungua pazia ikiwa kama ishara ya uwekaji wa jiwe la msingi ujenzi wa Nyumba za Makaazi ya Wanajeshi wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Vitongoji Wilaya ya Chake chake Pemba leo,ikiwa katika sherehe za shamra shamra za miaka 51 ya mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.
No comments:
Post a Comment