KATIBU Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu
wa serikali Dr. Servacius Likwelile, mchana wa leo ametiliana saini
makubaliano ya mkataba wa kuanzisha Mradi wa Maji katika Wilaya ya Same na
Mwanga.
Dr. Likwelile alisaini Mkataba huo kwa niaba ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mfuko wa maendeleo ya uchumi wa Kuwait . Aliye wakilisha Mfuko huo ni Bw. Abdulwahab A. Al- Bader ambaye ni Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko.
Dr. Likwelile alisaini Mkataba huo kwa niaba ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mfuko wa maendeleo ya uchumi wa Kuwait . Aliye wakilisha Mfuko huo ni Bw. Abdulwahab A. Al- Bader ambaye ni Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko.
Aidha
katika kutiliana saini Mkataba huo Dr. Likwelile alimueleza Bw. Abdulwahab A.
Al- Bader kuwa, Serikali ya Tanzania inatambua kuwa mfuko umetoa Dola za
Kimarekani milioni 34.0 sawa na shilingi Bilioni 56.10 za Kitanzania kwa ajili
ya kusaidia mradi wa maji katika Wilaya ya Same na Mwanga. Hivyo inatoa
shukrani zake za dhati kwa nchi ya Kuwait na hasa kwa mfuko huu wa maendeleo ya
kiuchumi.
“Msaada
huu tulioupata leo utaisaidia Serikali kutatua tatizo la maji katika wilaya ya
Same na Mwanga, hii inaonyesha ni jinsi
gani mfuko huu wa Kuwait unavounga mkono na kutekeleza jukumu zima la kushiriki
katika masuala ya kijamii na ya kiuchumi kwa nchi yetu ya Tanzania, hivyo
tunaomba muendelee kutusaidia”. Alisema Dr. Likwelile.
Dr.
Likwelile alimueleza Bw. Abdulwahab A. Al- Bader kuwa, kama anavyofahamu gharama za mapendekezo ya mradi mzima ni Dola
za Kimarekani million 110.43 na hii inahitaji
uchangiaji kutoka katika mifuko mingine kama BADEA, mfuko wa maendeleo wa
Saudia , Mfuko wa Kimataifa wa OPEC na
Serikali kuchangia fedha kusaidia mradi huu.
"Kwa hili sina wasiwasi nalo kwani ninafuraha kujua kwamba umeshakubaliana na ninaujasiri kuwa jitihada zako zitafanikiwa." Alisema.
"Kwa hili sina wasiwasi nalo kwani ninafuraha kujua kwamba umeshakubaliana na ninaujasiri kuwa jitihada zako zitafanikiwa." Alisema.
“Mradi
huu wa maji wq wilaya ya Same na Mwanga
unalenga kusaidia kuwepo kwa maji kwenye jamii mbalimbali zilizopo kwenye mradi
huo.” Aliongeza Dr.Likwelile.
Aliendelea
kusema kuwa,mradi huo utakapo kamilika :
(i)
utaongeza
kiwango cha watu wengi kuweza kupata maji safi na salama ya kunywa.
(ii)
Uchumi
wa Same na Mwanga utaimarika pamoja na hali ya afya kwa jamii nayo itakuwa
imara hasa kwa maeneo yale yanayoguswa na mradi.
(iii)
Hali
ya maisha ya watu wa Same na Mwanga itainuka.
“Mafanikio
ya ukamilishaji wa mradi huu ni muhimu sana kwa uchumi wa jamii na maisha bora
kwa watu wa wilaya ya Same na Mwanga”. Alisema Likwelile.
Dr. Likwelilie
alimalizia kwa kusema kuwa“Tanzania na Kuwait ni marafiki wa muda mrefu sana,
hivyo tutazidi kushirikiana na kuhakikisha kila kitu kinaenda sawa”.
Imetolewa
na:
Ingiahedi
Mduma
Msemaji
Wizara
ya Fedha
Washington
D.C
11/10/2014
No comments:
Post a Comment