TANGAZO


Tuesday, October 14, 2014

Shina la CCM Pamba Road laadhimisha kifo cha Baba wa Taifa kwa kufanya usafi maeneo ya Posta Mpya

Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Shina la wakereketwa la Pamba Road, Sophia Mbwile, akizungumza na wanachama wa tawi hilo, mara baada ya kufanya usafi wa mazingira kwenye maeneo ya shina hilo, Posta Mpya, Sar es Salaam leo katika kuadhimisha kifo cha Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Nyerere, Dar es Salaam leo. Katikati ni Mwenyekiti wa shina hilo, Sharik Choughule na kushoto ni Katibu wa Uchumi na Fedha Kata ya Kivukoni, Abdalla Ally Selle 'Sosi Malema. (Picha zote na Kassim Mbarouk-www.bayana.blogspot.com)
Baadhi ya wakereketwa wa Shina la Pamba Road, wakifurahia jambo wakati wa maadhimisho ya kumbukumbu ya kifo cha Baba wa Taifa, Hayati Julius Nyerere, Dar es Salaam leo.
Katibu wa Uchumi na Fedha Kata ya Kivukoni, Abdalla Ally Selle 'Sosi Malema, akizungumza wakati wa maadhimisho ya kumbukumbu ya kifo cha Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Nyerere kwenye Shina la wakereketwa la Pamba Road.
Katibu wa Uchumi na Fedha Kata ya Kivukoni, Abdalla Ally Selle 'Sosi Malema, akizungumza wakati wa maadhimisho ya kumbukumbu ya kifo cha Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Nyerere kwenye Shina la wakereketwa la Pamba Road. Kulia ni Mwenyekiti wa shina hilo, Sharik Choughule.
Baadhi ya wakereketwa wa Shina la Pamba Road, wakiwa kwenye mkutano wa maadhimisho ya kumbukumbu ya kifo cha Baba wa Taifa, Hayati Julius Nyerere, Dar es Salaam leo.
Wakereketwa wa Shina la Pamba Road, wakiwa kwenye mkutano wa maadhimisho ya kumbukumbu ya kifo cha Baba wa Taifa, Hayati Julius Nyerere, Dar es Salaam leo.
Baadhi ya wakereketwa wa Shina la Pamba Road, wakiwa kwenye mkutano wa maadhimisho ya kumbukumbu ya kifo cha Baba wa Taifa, Hayati Julius Nyerere, Dar es Salaam leo.
Katibu Mhamasishaji na Uenezi wa CCM Tawi la IFM, Pius Mpweza, akizunguma wakati wa maadhimisho hayo jijini leo. Wapili ni Katibu wa Uchumi na Fedha, Kata ya Kivukoni, Abdalla Ally Selle 'Sosi Malema', Mwenyekiti wa shina hilo, Sharik Choughule na Katibu wake, Sophia Mbwile.
Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Shina la wakereketwa la Pamba Road, wakifanya usafi wa mazingira, wakiongozwa na Mwenyekiti wao, Sharik Choughule (katikati), kwenye maeneo ya shina hilo, Posta Mpya, Dar es Salaam leo. Viongozi wa Shina hilo katika kuadhimisha Siku ya kumbukumbu ya Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Nyerere, wameunda kamati ya usafi itakayoshughulikia kusafisha mazingira katika maeneo mbalimbali ya jiji.
Wakereketwa wa CCM wa Shina la Pamba Road, wakisafisha mazingira kwenye maeneo ya shina hilo, ikiwa ni katika maadhimisho ya kumbukumbu ya kifo cha Baba wa Taifa, Hayati Julius Nyerere, Dar es Salaam leo.
Baadhi ya wakereketwa wa Shina la Pamba Road, wakisafisha mazingira kwenye maeneo ya shina hilo, ikiwa ni katika maadhimisho ya kumbukumbu ya kifo cha Baba wa Taifa, Hayati Julius Nyerere, Dar es Salaam leo.

No comments:

Post a Comment