KATIBU Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu
wa serikali Dr. Servacius Likwelile, mchana wa leo ametiliana saini
makubaliano ya mkataba wa kuanzisha Mradi wa Maji katika Wilaya ya Same na
Mwanga. Dr. Likwelile alisaini Mkataba huo kwa niaba ya Serikali ya Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania na Benki ya Kiarabu ya Maendeleo ya uchumi ya Afrika.
Aliye wakilisha Benki hiyo ni Eng. Yousef I. Al-Bassam ambaye ni Makamu wa Mwenyekiti na Mkurugenzi Msimamizi wa mfuko wa maendeleo wa Saudia.
Aliye wakilisha Benki hiyo ni Eng. Yousef I. Al-Bassam ambaye ni Makamu wa Mwenyekiti na Mkurugenzi Msimamizi wa mfuko wa maendeleo wa Saudia.
Aidha
katika kutiliana saini Mkataba huo Dr. Likwelile alimueleza Eng. Yousef I.
Al-Bassam kuwa Serikali ya Tanzania
inatambua kuwa BADEA imetoa Dola za
Kimarekani milioni 12.0 sawa na shilingi Bilioni 20.1 za Kitanzania kwa ajili
ya kusaidia mradi wa maji katika Wilaya ya Same na Mwanga. Hivyo inatoa
shukrani zake za dhati kwa BADEA kwa kusaidia kuchochea maendeleo ya Tanzania.
“Msaada
huu tulioupata leo utaisaidia Serikali kutatua tatizo la maji katika wilaya ya
Same na Mwanga, hii inaonyesha ni jinsi
BADEA unaunga mkono na kutekeleza jukumu zima la kushiriki katika masuala ya
kijamii na ya kiuchumi kwa nchi yetu ya Tanzania, hivyo tunaomba muendelee
kutusaidia”. Alisema Dr. Likwelile.
Dr.
Likwelile alimueleza Eng. Yousef I.
Al-Bassam kuwa, kama anavyofahamu gharama za mapendekezo ya mradi mzima ni Dola
za Kimarekani million 110.43 na hii inahitaji
uchangiaji kutoka katika mifuko mingine kama mfuko wa maendeleo wa Saudia ,
Mfuko wa Kimataifa wa OPEC na Serikali
kuchangia fedha kusaidia mradi huu.
"Kwa hili sina wasiwasi nalo kwani
ninafuraha kujua kwamba umeshakubaliana na ninaujasiri kuwa jitihada zako
zitafanikiwa". Alisema.
“Mradi
huu wa maji wq wilaya ya Same na Mwanga
unalenga kusaidia kuwepo kwa maji kwenye jamii mbalimbali zilizopo kwenye mradi
huo.” Aliongeza Dr. Likwelile.
Aliendelea
kusema kuwa,mradi huo utakapo kamilika :
(i)
utaongeza
kiwango cha watu wengi kuweza kupata maji safi na salama ya kunywa.
(ii)
Uchumi
wa Same na Mwanga utaimarika pamoja na hali ya afya kwa jamii nayo itakuwa
imara hasa kwa maeneo yale yanayoguswa na mradi.
(iii)
Hali
ya maisha ya watu wa Same na Mwanga itainuka.
“Mafanikio
ya ukamilishaji wa mradi huu ni muhimu sana kwa uchumi wa jamii na maisha bora
kwa watu wa wilaya ya Same na Mwanga”. Alisema Likwelile.
Dr. Likwelilie
alimalizia kwa kusema kuwa“Tanzania na Saudia ni marafiki wa muda mrefu sana,
hivyo tutazidi kushirikiana na kuhakikisha kila kitu kinaenda sawa”.
Hali ya
hewa ya mjini Washington Dc. ni mvua za vipindi na baridi kiasi.
Imetolewa
na:
Ingiahedi
Mduma
Washington
D.C
11/10/2014
No comments:
Post a Comment