TANGAZO


Friday, November 1, 2013

Chuo cha Bahari Dar es Salaam (DMI) chafanya mahafali yake ya 9

Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini Meja Generali Mstaafu Ligate Sande akitoa hotuba katikamahafali ya 9 ya Chuo cha Bahari Dar es Salaam (DMI). (Picha zote na Hussein Makame, Ofisa Habari, Idara ya Habari-MAELEZO)
Ndudu na jamaa wa wahitimu wakifuatilia hotuba ya Mwenyeki.
Baadhi ya wahitimu katika ngazi mbalimbali wakimsikiliza Mwenyekiti wa bodi ya Chuo.
Mgeni Rasmi katika Mahafali ya 9 ya DMI Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Dk. Shaabani Mwinjaka akihutubia katika mahafali hayo.
Baadhi ya wahitimu katika ngazi mbalimbali wakimsikiliza Mgeni Rasmi katika Mahafali ya 9 ya DMI Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Dk. Shaabani Mwinjaka wakati alipokuwa akihutubia katika mahafali hayo.
Baadhi ya wahitimu katika ngazi mbalimbali wakimsikiliza Mgeni Rasmi katika Mahafali ya 9 ya DMI Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Dk. Shaabani Mwinjaka wakati alipokuwa akihutubia katika mahafali hayo.
Baadhi ya wahitimu katika ngazi mbalimbali wakimsikiliza Mgeni Rasmi katika Mahafali ya 9 ya DMI Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Dk. Shaabani Mwinjaka wakati alipokuwa akihutubia katika mahafali hayo.
Baadhi ya wahitimu katika ngazi mbalimbali wakimsikiliza Mgeni Rasmi katika Mahafali ya 9 ya DMI Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Dk. Shaabani Mwinjaka wakati alipokuwa akihutubia katika mahafali hayo.
Mgeni Rasmi Dk. Mwinjaka akimtunuku Cheti Mhitimu wa Stashahada ya Juu ya Usafirishaji wa Majini (ADMT), Dilshad Murtaza kwa kupata Daraja la Kwanza la GPA 4.5 kwenye Kozi hiyo.
Naibu Makamu Mkuu wa Chuo, Mipango, Fedha na Utumishi, Dk. Tumaini Gurumo akimkabidhi Mgeni Rasmi zawadi aliyoandaliwa na chuo hicho.

Hussein Makame, MAELEZO
CHUO cha Bahari Dar es Salaam (DMI), kimejipanga kutoa elimu ya rasilimali za baharini ikiwemo mafuta na gesi katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati na dunia kwa ujumla.

Hayo yamesemwa leo na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa DMI, Meja Generali Mstaafu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ); Ligate Sande katika mahafali ya 9 ya chuo hicho, yaliyofanyika jijini Dar es Salaam leo.

Mwenyekiti huyo, alisema wamefikia hatua hiyo ili kuifanya Tanzania ambayo ni nchi iliyoko ukanda wa bahari wenye wingi wa rasilimali ya mafuta na gesi kunufaia na rasilimali hizo.

Alisema moja ya kigezo cha kuboresha na kusimamia rasilimali baharini na maeneo yanayozunguka bahari ni kuwa na rasilimali watu ya kutosha na yenye ujuzi na weledi katika mambo ya bahari.

Meja General Mstaafu Sande alisema pamoja na kuwa na rasilimali watu ya kutosha kunahitajika mikakati ya makusudi ili  kuifanya Sekta ya bahari iwe endelevu na yenye tija kwa Taifa.

“DMI imejipanga katika kutoa elimu ya aina hii katika ukanda huu wa Afrika Mashariki na kati na dunia kwa ujumla” alisema mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa chuo hicho ambacho ni Kituo cha Ubora (Centre of Excellency) wa Elimu ya Bahari inayotambuliwa na Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Akizungumzia changamoto zinazikikabili chuo hicho, mwenyekiti huyo alisema pamoja na changamoto nyingine, DMI kina uhaba wa miundombinu ya madarasa na ofisi za walimu katika kukidhi mahitaji ya ongezeko la wanafunzi wanaojiunga na chuo hicho kutoka nchi mbalimbali barani Afrika.

Akizungumzia changamoto hizo, Mgeni Rasmi kwenye Mahafali hayo Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi Dk. Shaaban Mwinjaka alisema anatambua umuhimu wa DMI na changamoto zinazokikabili.

“Hata hivyo ninatambua kuwa DMI inao uwezo wa kutoa mchango wa wataalamu katika fursa hizo hususan waendesha meli, Wahandisi wa meli, Uchimbaji gesi na Mafuta, Usafirishaji shehena, Ukarabati wa meli, Ajira ndani na nje ya nchi” alisema Dk Mwinjaka.

Katika mahafali hiyo yenye kauli mbiu isemayo Sekta ya Bahari “Matokeo Makubwa Sasa” Zingatia Elimu Bora na Usawa Kijinsia”, yalishuhudia wahitimu 403 wakitunukiwa vyeti kwa ngazi ya Stashahada ya Juu, Stashahada na Cheti.

Mbali na tunu hizo, wahitimu 10 walitunukiwa vyeti kutokana na kufanya vizuri kwenye masomo katika mwaka wa masomo wa 2011/2012 na 2012/2013 akiwemo Dilshad Murtaza aliyepata Daraja la Kwanza la ufaulu wa GPA ya 4.5 katika Shahada ya Juu ya Usafirishaji wa Majini (ADMT).

No comments:

Post a Comment