TANGAZO


Tuesday, July 10, 2012

Makamu wa Rais wa Afrika Kusini atembelea Mazimbu, Morogoro

Makamau wa Rais wa Afrika Kusini, Kgalema Motlanthe (katikati), akiangalia moja ya makaburi ya wapigania Uhuru (ANC), eneo la Mazimbu, mjini Morogoro jana.
 
Makamu wa Rais wa Afrika ya Kusini, Kgalema Motlanthe, Julai 9, mwaka huu alifanya ziara ya siku moja Mjini Morogoro, ililiyokuwa mahusisi kwa ajili ya kutembelea eneo la Mazimbu, iliyokuwa kambi ya wapingania uhuru wa Chama cha ANC.
Ziara hiyo ilikuwa ni sehemu ya kuadhimisha miaka 20 tangu harakati za ukombozi wa Afrika Kusini zilipomalizika, katika Kambi hiyo, ANC iliacha majengo na vitu mbalimbali vilivyokabidhiwa Serikali ya Tanzania, pia yapo makaburi kadhaa walimozikwa mashujaa hao, ambapo Makamu huyo wa Rais aliweza kuzuru na kuweka shada la maua katika mnara wa kumbukumbu ya wapigania uhuru hao pamoja na kupanda mti.
Kabla ya kufanya shughuli hiyo,alipata fursa ya kutembezwa maneo mbalimbali yakiwemo majengo yaliyokuwa yakitumiwa na wapigania uhuru hao, ikiwemo Shule ya Msingi na Awali, Shamba la Mifuko, Kiwanda cha samani pamoja na Hospitali .
Makamau wa Rais wa Afrika Kusini, Kgalema Motlanthe, akitoa heshima baada ya kuweka shada la maua kwenye moja ya makaburi ya wapigania Uhuru wa ANC, eneo la Mazimbu mjini Morogoro.
 
Makamau wa Rais wa Afrika Kusini, Kgalema Motlanthe, akipanda mti eneo la Makaburi ya Wapigania Uhuru wa ANC, Mazimbu mjini Morogoro jana.
 
Makamau wa Rais wa Afrika Kusini, Kgalema Motlanthe, akitoka kutembelea hospitali ya Mazimbu, ambayo ilikuwa ikitumiwa na wapigania Uhuru wa ANC, ambapo kwa sasa imekarabatiwa na kuongezwa majengo mapya.
 
 Baadhi ya raia wa Afrika Kusini walioambatana na Makamu wa Rais wa nchi hiyo hapa nchini jana.
 
Burudani kwa mgeni rasmi, Makamau wa Rais wa Afrika Kusini, Kgalema Motlanthe, alipotembelea Shule ya Msingi ya Chief Albert , Mazimbu mjini Morogoro jana. (Picha zote na mdau wetu)

No comments:

Post a Comment