TANGAZO


Thursday, March 22, 2018

Tetesi za soka Ulaya Alhamisi 22.03.2018

Manchester United inapanga kumsajili beki wa Real Madrid Raphael Varane, 24, kwa dau la £50m. (Mirror)

Image captionManchester United inapanga kumsajili beki wa Real Madrid Raphael Varane, 24, kwa dau la £50m. (Mirror)
Manchester United inapanga kumsajili beki wa Real Madrid Raphael Varane, 24, kwa dau la £50m. (Mirror)
Jose Mourinho hakufurahia kitendo cha ukosefu wa nidhamu cha kiungo wake wa kati Paul Pogba wakati alipoingilia kati mahojiano ya runinga ya mkufunzi huyo kufuatia ushindi wa 2-1 dhidi ya Liverpool mapema mwezi huu. (Sun)
Image captionChelsea imejiunga katika harakati za kumsajili beki wa Tottenham Toby Alderweireld, 29,
Chelsea imejiunga katika harakati za kumsajili beki wa Tottenham Toby Alderweireld, 29, ambaye anaweza kuondoka katika klabu hiyo kwa malipo ya £25m yaliowekwa katika kandarasi yake.(Mirror)
Kiungo wa kati wa Liverpool Emre Can, 24, anasema kuwa anataka kuchezea klabu kubwa msimu ujao. Kandarasi ya raia huyo wa Ujerumani Anfield inakamilika mwisho wa msimu huu.(Suddeutsche Zeitung, via Liverpool Echo)
Image captionKiungo wa kati wa Liverpool Emre Can, 24,
Ili kuchukua mahala pake Can, Liverpool wanaamini kwamba watamsajili kiungo wa kati wa Napoli Jorginho 26 ambaye anadaiwa kuwa na thamani ya £50m. (Mirror)
Arsenal italazimika kulipa dau la £35m iwapo inataka kumsajili beki Ruben Dias, 20, kutoka klabu ya Ureno Benfica. (Record, via Football London)
Image captionbeki Ruben Dias, 20, kutoka klabu ya Ureno Benfica
Mkufunzi wa Southampton Mark Hughes anataka kumsajili kiungo wa kati Xherdan Shaqiri, 26, kutoka Stoke kwa dau la £20m. (Star)
Everton inachunguza hali ya beki wa kushoto Luke Shaw katika klabu ya Manchester United na tayari walituma maskauti wake kumtazama mchezaji huyo 22 katika kombe la FA dhidi ya Brighton. (ESPN)
Image captionJack Wilshere
Kiungo wa kati wa Besiktas Oguzhan Ozyakup, 25, anatarajiwa kujiunga na Everton katika uhamisho wa bure mwisho wa msimu huu iwapo timu hiyo ya Merseyside itashindwa kumsajili kiungo wa kati wa Arsenal Jack Wilshere, 26. (Turkish-Football.com)
Burnley itajiunga katika harakati za kumsaka beki wa West Brom Craig Dawson, 27, kwa dau la £10m iwapo timu hiyo itashushwa daraja. Aston Villa na Middlesbrough pia wanamsaka mchezaji huyo. (Mirror)
Image captionReal Madrid wamekubali ombi la dau la £113m la winga Gareth Bale, 28, kutoka klabu ya ligi ya China
Real Madrid wamekubali ombi la dau la £113m la winga Gareth Bale, 28, kutoka klabu ya ligi ya China , lakini raia huyo wa Wales anataka kuondoka katika klabu hiyo ya La Liga iwapo atajiunga na klabu nyengine kubwa Ulaya.(Diario Gol - in Spanish)
Barcelona itawatuma maskauti wake kumchunguza kinda wa Ajax Matthijs de Ligt, 18, wakati mchezaji huyo wa Uholanzi atakaposhiriki katika mechi ya kirafiki dhidi ya Uingereza na Ureno. Mundo Deportivo - in Spanish)
Image captionAtletico Madrid italazimika kulipa dau la £105m kumsajili mshambuliaji Paulo Dybala, 24, kutoka Juventus. (Mail)
Atletico Madrid italazimika kulipa dau la £105m kumsajili mshambuliaji Paulo Dybala, 24, kutoka Juventus. (Mail)
Reading inapanga kumsajili mkufunzi wa zamani wa Swansea Paul Clement na Steve Cotterill, aliyeifunza Birmingham hivi majuzi , kuchukua mahala pake Jaap Stam ambaye alipigwa kalamu siku ya Jumatano. (Sky Sports)
Image captionMshambuliaji wa zamani wa Real Madrid Raul anatarajiwa kuwa kocha wa vijana katika klabu hiyo. (Marca)
Mshambuliaji wa zamani wa Real Madrid Raul anatarajiwa kuwa kocha wa vijana katika klabu hiyo. (Marca)
Nyota wa zamani wa Barcelona Ronaldinho anatarajiwa kuwania ubunge katika taifa lake la Brazil. (Mail)

No comments:

Post a Comment