TANGAZO


Thursday, November 23, 2017

Raia wa Uingereza aliyeiomba mahakama imfunge''

Bradley Grimes

Image captionTabia ya Bradley ya hali ya kutopenda maisha ya kijamii ilimzuwia ''kuzurura" karibu na maeneo ya biashara
Baada ya kupigwa marufuku kuomba na kulala ovyo ovyo kwenye veranda za maduka katika mji wa Middlesbrough, Bradley Grimes alimuomba jaji wa mahakama ammpeleke gerezani kuliko kumuacha bila makazi .
Itakuwa na athari gani? " Kile walichokifanya ni kunifanya nisipende kuishi katika jamii kujaribu kunizuwia nisiwe omba omba.
Lakini lazima niombe ili kuweza kuishi," Bradley Grimes alimueleza mwandishi wa BBC.
Alikosa makazi ya kuishi baada ya kuondoka kwenye mfumo wa misaada ya jamii akiwa na umri wa miaka 17.
Bradley Grimes mwenye tatizo la kigugumizi na ''akili ya kitoto'' hakuweza kupata kazi na mara kwa mara amekuwa omba omba- akiwaomba wasafiri chakula na pesa kando ya mtaa wenye shughuli nyingi.
Image captionHapa ndipo Bradley anasema hulala mara kwa mara, kando kidogo ya bara bara yenye shughuli nyingi
Lakini hii ilimfanya jaji katika mahakama ya Middlesbrough kumuamrisha kuacha tabia hiyo
Amri hiyo iliambatana na amri ya kumzuwia " kuzurura" nje ya majumba ya biashara.
Bradley anasema amri hiyo ilimzuwia "kukaa nje ya duka " na kulala kwenye bveranda za maduka ambako alikuwa akipata joto, na hilo lilimfanya kuendelea kukamatwa na maafisa wa usalama.
" mitambo ya kamera ya CCTV inachukua picha na kuituma moja kwa moja kwa polisi au walinzi wa mitaa. Polisi wakija, unakamatwa ," alieleza Bradley, ambaye sasa ana umri wa miaka 23.
Anasema kilichomfanya maafisa wa usalama ni kukaamkabala ni kituo cha basi.
Image captionBradley anasema kuwa wakati mmoja alikamatwa alipokuwa ameketi mkabala na kituo cha basi
"Nilifika kwenye kituo ambako walinifunga mara moja ama mara mbili kwa siku, katika kipindi cha miezi michacheg
"Nilikuwa nafungwa zaidi nyakati za mwishoni mwa juma.
"Siwezi hata kukaa kwenye kiti cha umma bila kutiwa nguvun. Inabidi nishinde nikizurura ."Kutokana na kuchoshwa na hali hii, aliamua kuomba msaada usio wa kawaida at his situation, he decided to seek .
Alipokuwa mahakamani, akishtakiwa kwa kukiuka hukumu ya kifungo cha nyumbani cha miezi minne- kosa mabalo alikiri kulifanya - alimuomba jaji kumuweka jela,.

No comments:

Post a Comment