Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye (kushoto) akizungumza na Mkurugenzi Mkuu wa Makao Makuu ya Kampuni ya Startimes kutoka nchini China Bw. Pang XinXing (katikati) kuhusu kurejea mkataba wa TBC1 na kampuni hiyo kwa lengo la kufanya maboresho ya mkataba leo Septemba 30, 2016 ofisini kwake jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye (kulia) akimsikiliza mkalimani wa Mkurugenzi Mkuu wa Makao Makuu Kampuni ya Startimes kutoka China Bi. Yuan Li Shan (kushoto), pale uongozi huo wa juu ulipofika ofisini kwake kueleza mikakati ya kuboresha Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC1), Septemba 30, 2016.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye (kulia) akipokea zawadi kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa Makao Makuu ya Kampuni ya Startimes kutoka China Bw. Pang Xin Xing (kushoto) alipomtembelea ofisini kwake jijini Dar es Salaam leo Septemba 30, 2016, kuzungumzia mikakati ya kuendeleza Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC 1) jijini.
No comments:
Post a Comment