TANGAZO


Saturday, March 19, 2016

Mitt Romney:Cruz ndiye atakayemzuia Trump

Mitt Romney
Aliyekuwa mgombea wa urais nchini Marekani Mitt Romney amesema kuwa atampigia kura seneta wa Texas Ted Cruz kwa kuwa ''havutiwi'' na mgombea wa chama hicho aliye kifua mbele Donald Trump.
Donald Trump na Mitt Romney
Alifanya kampeni na Gavana John Kasich huko Ohio lakini akasema kuwa kumpigia kura Bwana Cruz ndio nijia ya kipekee kumzuia Trump.
Anajiunga na viongozi wengine wa Republican wanaomuunga mkono Bwana Cruz.
Ted Cruz
Bwana Trump ameshinda majimbo mengi na kwa sasa ana takriban wajumbe 678 huku akitakiwa kujipatia wajumbe 1237 kushinda uteuzi huo.

No comments:

Post a Comment