TANGAZO


Sunday, March 27, 2016

Mali yakamata 2 waliopanga ugaidi Ivory Coast

Image copyrightReuters
Image captionMali yakamata watu 2 waliopanga ugaidi Ivory Coast
Polisi nchini Mali wanasema watu wawili wamekamatwa kaskazini mwa nchi, kwa kuhusika na shambulio lilofanywa mwezi huu na Al Qaeda, katika eneo la watalii nchini Ivory Coast.
Mmoja wao anasemekana kuwa ndiye aliyepanga usafiri wa washambuliaji.
Mwenzake anatuhumiwa kuwa mshauri mkuu kiongozi wa njama hiyo.
Wanaume wote wawili ni raia wa Mali.
Image copyright
Image captionWatu 19 waliuwawa pale wanaume waliokuwa wamejihami kwa silaha kali kuingia kwa nguvu katika eneo la pwani, la Grand Bassam
Watu 19 waliuwawa pale wanaume waliokuwa wamejihami kwa silaha kali kuingia kwa nguvu katika eneo la pwani, la Grand Bassam, karibu na mji mkuu, wa Ivory Coast, Abidjan.
Waliwapiga risasi waliokuwa wakikoga ufukweni, kabla ya kuivamia hoteli.

No comments:

Post a Comment