TANGAZO


Monday, May 18, 2015

Tanzania na Msumbiji kushirikiana zaidi kuboresha hali ya uchumi wa nchi hizo

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete (kulia) akiwa na mgeni  wake Rais wa Msumbiji Mhe. Filipe Nyusi katika dhifa ya kitaifa iliyofanyika jana usiku Ikulu jijini Dar es Salaam. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete akihutubia kwenye dhifa.
Rais wa Msumbiji Filipe Nyusi akizungumza. 
Baadhi ya Maofisa Balozi waliohudhuria dhifa wakibadilishana mawazo. 
Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba  akibadilishana mawazo na baadhi ya viongozi na wageni waalikwa katika hafla hiyo. Wa pili kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Raymond Mushi na kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji (TIC) Julieth Kairuki. 
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe. Paul Makonda (kushoto) akiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Sekta Binafsi (TPSF), Godfrey Simbeye na Mbunge wa Singida Mjini (CCM) Mohamed Dewji na Mfanyabiashara Maarufu nchini Yusuph Manji. 
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadiki akizungumza na Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete, akisalimiana na baadhi ya viongoz wa Serikali ya Msumbiji. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete, akizungumza na Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF) Profesa Ibrahim Lipumba. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete, akisalimiana na Mnadhimu Mku wa Majeshi , Samuel Ndomba. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete (katikati mwenye tai nyekundu) akiwa na mgeni wake Rais wa Msumbiji Filipe Nyusi wakifurahia burudani ya kikundi cha ngoma baada ya kumalizika kwa dhifa ya Kitaifa iliyofanyika Ikulu jijini Dar es  Salaam. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete, akumuongoza mgeni wake kutoka nje ya ukumbi wa Ikulu. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete, akimuaga mgeni wake. (Picha na Hussein Makame-MAELEZO)

Na Magreth Kinabo – Maelezo
TANZANIA na Msumbiji zimekubaliana kushirikiana kiuchumi,  ili kuweza kuboresha  hali ya uchumi kwa manufaa ya nchi hizo pamoja na watu wake.

 Hayo yalisemwa  jana wakati wa hafla ya  dhifa ya kitaifa iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaama ambayo  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Jakaya Mrisho Kikwete alimuandalia mgeni wake Rais wa Msumbuji  Mhe. Filipe Nyusi.
Akizungumzia kuhusu   ziara  yake   Rais Nyussi alisema kuwa amefurahishwa na mapokezi aliyoyapata  na kuongeza kwamba  ujio  huo utaendeleza ushirikiano wa kiuchumi baina ya nchi hizo mbili kupitia  nishati ya gesi.

“Nina imani kwamba tutaweza kushirikiana kiuchumi  ili kuendeleza ushirikiano wetu hususani kupitia  nishati ya gesi,” alisema Rais Nyusi.

Rais Nyusi  aliongeza kwamba   ili kuweza kupata mafanikio ya kiuchumi zaidi upo umuhimu wa kuimarisha viwanda kwa kuvisaidia viwanda vya kati na vidogo. 

 Kwa upande wake  Rais Kikwete alisema ujio wa Rais Nyusi ni ishara ya kuingia katika hatua nyingine  ya ushirikiano baina ya nchi hizo mbili   kutokana na kwamba wamekubaliana  kushirikiana katika utoaji visa , masuala ya kiuchumi kupitia gesi,    kielimu,  ulinzi na usalama , ikiwemo  kuendeleza  biashara na uwekezaji .

Rais Kikwete aliongeza kuwa  anatarajia kumaliza muda wa uongozi wake  huku uhusiano wa nchi hizo ukiwa  katika hali nzuri   na anatagemea kwamba utaendelea  kuwa imara hata atakapomaliza muda wake.  

Rais Nyusi yupo hapa nchini kwa  ziara yake  ya siku tatu ikiwa ni ya kwanza kuifanya nchi za nje tangu alipochaguliwa kushika madaraka ya nchi hiyo.


No comments:

Post a Comment