TANGAZO


Monday, May 18, 2015

Butiku Kufanya Mkutano na Viongozi Wakuu wa Kitaifa, Wazee Kujadili Amani na Umoja wa Taifa

Mkurugenzi  Mtendaji wa  Taasisi ya Mwalimu Nyerere Foundation Bw. Joseph Butiku, akizungumza na waandishi wa habari, Dar es Salaam leo kuhusu mkutano wa Viongozi Wakuu wa Kitaifa, Wazee pamoja na viongozi wa Vyama na Taasisi mbalimbali nchini. Kulia ni Msaidizi wa Mkurugenzi huyo, Gallus Abedi. (Picha zote na Kassim Mbarouk-www.bayana.blogspot.com) 
Mkurugenzi  Mtendaji wa  Taasisi ya Mwalimu Nyerere Foundation Bw. Joseph Butiku, akifafanua jambo kwa waandishi wa habari, wakati wa mkutano huo jijini leo.
Mkurugenzi  Mtendaji wa  Taasisi ya Mwalimu Nyerere Foundation Bw. Joseph Butiku, akiwaonesha waandishi wa habari, baadhi ya nyaraka zenye mawazo yaliyotolewa na viongozi mbalimbali pamoja na wazee walikutana nao.
Baadhi ya waandishi wa habari, waliokuwepo kwenye mkutano huo, wakimsikiliza na kunukuu maelezo yaliyokuwa yakitolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere Foundation Bw. Joseph Butiku, wakati wa mkutano huo jijini leo.

Na Anitha Jonas – MAELEZO.
Tarehe: 18/05/2015.
TAASISI ya Mwalimu Nyerere Foundation imeandaa  mkutano wa mashauriano unaotarajia kufanyika tarehe Mei 19-20 mwaka huu, ambapo watajadili mambo mbalimbali kuhusu Amani na Utulivu wa nchi ya Tanzania.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi  Mtendaji wa  Taasisi ya Mwalimu Nyerere Foundation Bw. Joseph Butiku alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es  Salaam kuhusu maandalizi ya mkutano  huo na agenda za mkutano huo.

“Mkutano huu utahusisha viongozi wakuu wa Serikali  ikiwemo walioko madarakani na waliokwisha kustaafu,viongozi wakuu wa  Siasa na viongozi wa wakuu wa Dini na lengo kuu la kushirikisha viongozi  hao ni kutafakari na kujadili hali ya amani,umoja,na utulivu wanchi yetu kwa kuzingatia kuwa viongozi hao ndiyo wenye jukumu na wajibu wa kwanza wa kusimamia amani na umoja”, alisema Bw.Butiku.

Mbali na hayo Bw.Butiku aliendelea kusema mkutano huo utajadili hoja mbalimbali  ikiwemo masuala ya ukosefu ya ajira kwa vijana,kutoa ufafanuzi wa kuhusu Muungano,muongozo wa elimu kwa taifa letu pamoja na uanzishwaji wa vikundi vya ulinzi ndani ya vyama vya siasa.

Aidha hoja hizo ziliwasilishwa kwa wadau hao watakaoshiriki mkutano huo kwa ajili ya kutoa mapendekezo yao juu ya  hoja hizo na zaidi ya washiriki kumi na nne wametoa mapendekezo yao katika hoja hizo na zitakazojadiliwa
.
Kwa upande mwingine Bw.Butiku alisema muasisi  ya Mwalimu Nyerere Foundation  Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alianzisha taasisi hiyo kwa lengo la kusimamia mwenendo wa amani na umoja kwa taifa na hivyo ndiyo maana wameandaa mkutano huo ilikujadili hatma ya taifa baada ya kuona uwepo kwa viashiria vinavyotishia amani na umoja. 

Hata hivyo mkutano huo unatarajiwa kuwahudhiriwa na viongozi mbalimbali wakisiasa na wadini akiwemo Bw. Ibrahimu Lipumba (CUF), Bw. Wilbroad Slaa (CHADEMA), Bw.James Mbatia (NCCR) na Katibu wa Chama cha Mapinduzi Taifa Bw.Abraham Kinana, Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara Bw. Philip Mangula, Katibu Mwenezi (CCM) Bw. Nape Nauye na viongozi wa dini ni uongozi.

No comments:

Post a Comment