TANGAZO


Friday, April 3, 2015

Zimbabwe:ZANU-PF chamtimua Bi Mujuru

Bi Joice Mujuru
Aliyekuwa makamu wa rais nchini Zimbabwe Joice Mujuru amefukuzwa katika chama tawala ZANU-PF.
Chama hicho kinasema alipanga njama za kumuondoa mamlakani rais Robert Mugabe mbali na kukiharibia jina chama hicho- madai ambayo ameyakana hapo mbeleni .
Bi Mujuru alipigana vita vya Guerilla pamoja na Mugabe miaka ya sabini dhidi ya uongozi wa weupe na alionekana kama mrithi wake,kabla ya kukosana naye mwaka uliopita swala lililomfanya kufutwa kazi kama makamu wa rais mnamo mwezi Disemba.
Waandishi wanasema alishtumiwa sana na mke wa Mugabe, Grace ambaye anaongoza wanawake katika chama hicho.

No comments:

Post a Comment