Waziri wa Fedha Mhe. Saada Salum akifuatilia kwa makini maswali aliyokuwa akiulizwa na Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Dunia Tanzania, Rwanda, Uganda na Burundi Bw. Philippe Dongier (hayupo kwenye picha). Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha Zanzibar.
Ujumbe wa Mkutano huo kutoka pande zote mbili yaani Tanzania na Benki ya Dunia, wakimsikiliza kwa makini Mchumi mwandamizi kutoka Benki ya Dunia.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu wa Serikali Dr. Servacius Likwelile akijadiliana jambo na Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Dunia Tanzania, Rwanda, Uganda na Burundi Bw. Philippe Dongier kabla ya kikao kuanza rasmi.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu wa Serikali Dr. Servacius Likwelile (wapili kushoto), akiandika kwa makini hoja na mapendekezo yaliyokuwa yakitolewa na Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Dunia Tanzania, Rwanda, Uganda na Burundi Bw. Philippe Dongier.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu wa Serikali Dr. Servacius Likwelile
akijibu na
kueleza kwa umakini hoja na mapendekezo yaliyokuwa yametolewa na Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Dunia
Tanzania, Rwanda, Uganda na Burundi Bw. Philippe Dongier.
WAKATI Tanzania ikiendelea kupambana na umaskini , Benki ya Dunia imesema kuwa,”
tumefurahishwa sana na mwenendo mzuri wa usimamizi wa fedha na bajeti”. Hayo
yalisemwa na Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Dunia Tanzania,
Rwanda, Uganda na Burundi Bw. Philippe Dongier katika mkutano ambao waziri wa
Fedha Mhe. Saada Mkuya Salum alikuwepo.
Mambo
mbalimbali yalizungumziwa katika mkutano huo ambapo suala la upatikanaji wa fedha kusaidia bajeti ya
serikali lilipewakipaumbele.Maboresho katika Sekta ya umeme nalo jambo mojawapo liliopewa uzito
kwani Nchi wahisani wamepata moyo wakuachia misaada baada ya kuona Serikali
imeweza kulishughulikia suala zima la IPTL.
“
Nchi wahisani wamekubali kuendelea kutoa misaada kwa asilimia mia, hii ni kwa
sababu tu! serikali yenu imekubali kuchukua hatua dhidi ya tatizo la IPTL”, alisema Philippe.
Akizungumza
na waandishi wa habari Mhe. Mkuya alisema kuwa, suala la kuboresha Pension nalo
lilizungumziwa na chombo hiki kitasaidia serikali katika kuboresha malipo ya
uzeeni (pension) na kuwezesha mashirika ya “pension” ili yaweze kuwa na uwezo
wa kusaidia wastaafu. Aidha tumekubaliana
kuwa watatusaidia katika suala zima la kuboresha uwazi serikalini na
mazingira ya biasha Tanzania.Aliongeza Mkuya.
Jambo
lingine lililochukua uzito katika majadiliano hayo ni suala la kufanya ukaguzi
Bandarini. Hili limejitokeza baada ya kubainika kuwa kuna baadhi ya wafanya
biashara sio waaminifu hivyo benki ya Dunia imeitaka Serikali kuangalia upya
maamuzi ya mwanzo ya serikali yakuto kagua mizigo, na kusema kuwa wanasubiri majibu
juu ya kubadilisha utaratibu wa mwanzo.
Tanzania imekubali kukaa kwa pamoja Wizara
na Fedha na TRA ili kurudisha majibu na mkakati ambao kama serikali watakuwa
wamekubaliana.
“Kumekuwa
na madai mengi ambayo yanadaiwa na makandarasi na wafanyabiashara wadogo,
tutajitahidi kuyalipa iliyaishe lakini kwa wale wenye nyaraka halali, tunaenda
kupiga marufuku kwa Afisa masuuli wote kuwa kuanzia sasa hakuna kufanya malipo
yoyote kama hakuna fedha kwa ajili ya shughuli hiyo”.Alisema Mkuya.
“
Hii itasaidia kupunguza madeni. Ninasema haya kwani ndicho kitu
tulichokubaliana kwenye mkutano huu”. Alisistiza Mkuya.
Mikutano
hiyo bado inaendelea hapa mjini Washington DC. Hali ya hewa ni baridi kiasi.
Imetolewa na Msemaji :Wizara ya fedha
Ingiahedi C.Mduma
Washington DC
16/04/2015
No comments:
Post a Comment