Waziri wa Habari Vijana Utamaduni na Michezo Mhe. Fenella Mukangara akisoma Muswada wa Baraza la Vijana ndani ya ukumbi Bunge, Mjini Dodoma. (Picha na Anitha Jonas – MAELEZO, Dodoma)
Na Anitha Jonas –
MAELEZO,Dodoma.
SERIKALI inatarajia kuanzisha
Baraza la Vijana litakalo kuwa chombo cha vijana kitakacho waunganisha Kitaifa
bila kujali itikadi zao za Kisiasa,Imani zao za Kidini wala tofauti zao za Rangi,hayo yamesemwa na Waziri
wa Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo Mhe.Fenella Mukangara alipokuwa akisoma
Muswada wa Sheria ya Baraza la Vijana Tanzania Bungeni Mjini Dodoma.
Mheshimiwa Mukangara
aliendelea kusema Baraza hilo litaisaidia Serikali kuweza kuwafikia vijana kwa
urahisi na kusikiliza shida zao pamoja na kutoa ufumbuzi wa hoja mbalimbali za
vijana.Hata hivyo chimbuko la Muswada
huo ni katika kutekeleza Sera ya Taifa ya Maendeleo ya Vijana ya 2007,Ibara ya
3 Sehemu ndogo ya 11 inayosema kwa uwazi Serikali itawezesha kuundwa kwa Baraza
Baraza la Vijana na kuanzisha mfumo wa kisheria ili kuliwezesha kufanya kazi.
“Madhumuni ya Muswada huu ni
Kutunga Sheria ya Baraza la Vijana Tanzania(The Youth Council of Tanzania 2015)
ili kuwa na chombo cha Kitaifa cha kuwewezesha vijana kujadili masuala
yao,kutambua majukumu yao,kukuza maadili mema,kukuza moyo wa umoja
,uzalendo,uwajibikaji na kujitolea kwa malengo chanya miongoni mwao katika nchi
yetu,”alisema Mhe.Mukangara.
Mbali na hayo katika sehemu
ya pili kifungu cha 4-15 cha Muswada huo unaeleza juu ya masharti mbalimbali
kuhusu Uanzishwaji,Uanachama,Muundo na kazi za Baraza.Pia sehemu hii imefafanua
Mamlaka ya Baraza na vyombo vya utendaji katika ngazi ya Taifa,Mkoa na Wilaya.
Aidha, kwa upande wa maoni ya
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii yaliyosomwa na Mwenyekiti wake
Said Mtanda aliishauri Serikali katika kifungu cha 4(3)Kisomeke Uanachama
utakuwa na uwazi na hiari kwa kijana yeyote mwenye umri wa kuanzia miaka 15 mpaka 35.Pia kifungu cha
4(4) imeeleza kuwa baraza halitakuwa kisiasa liongezwe neno halitakuwa na
Itikadi za Kidini.
Katika kipindi cha
majadiliao ya Muswada huo naye Mhe.Kuluthum Mchuchuri (Mb) Viti Maalum CUF aliipongeza Serikali kwa
mchakato wake mzuri wa kuandaa Baraza la Vijana litakalo saidia vijana kujadili
matatizo yao na kuyawasilisha Serikali kwa kupatiwa ufumbuzi kwa urahisi,pia
ameishauri Serikali katika suala la wajumbe
uwawakilishi waanze kuanzia ngazi ya Kata na Serikali pia iweke wazi ni
kwa utaratibu gani wawakilishi hao watapatikana.
Naye Mhe.Magret Sitta Mbunge
wa Viti Maalum CCM aliiomba Serikali kuandaa ziara kwenda kuangalia mabaraza ya
Vijana katika nchi za wenzetu
yanafanyaje kazi na kujifunza,pia aliendelea kuiomba Serikali itoe mafunzo
mbalimbali ya ufundi kwa kushirikia na taasisi ya Veta na Vyuo vya Wananchi
ilikuwapatia elimu itakayo wasaidia vijana kujikwamua kiuchumi na kupunguza
idadi ya vijana wa vijiweni.
Pamoja na hayo naye Mbunge
wa Kasulu Mjini (NCCR) Mhe. Moses Machali alishauri Serikali Kuanzisha asasi
moja ambayo vijana watakayo jiunga huko ili kudhibiti uanzishwaji wa asasi
bandia kwa watu wenye nia ya kujinufaisha,pia aliipongeza Serikali kwa kuleta
Muswada huo kwani unamanufaa Makubwa kwa vijana.
Aidha,mbali ya kuwepo na
marekebisho mbalimbali ya Muswada huo Serikali iliyapokea maombi ya Suala la
Baraza hilo kuanzia katika ngazi ya Kata ilikupata uwakilishi uliyowa uhakika
na baraza likalete manufaa kwa kuanzia ngazi ya chini ambapo ndipo vijana wengi
wanapatikana na jamii inawafahamu kwa usahihi zaidi.
Halikadhalika Serikali
iliridhia kuanzishwa kwa uwakilishi wa vijana watano kutoka kundi maalum kwa
maana ya wenye ulemavu na ili kuweka uwianao wa vijana hawa kuweza kuwasilisha
maombi yao kwa Serikali kwa urahisi huku ikizingatia mahitaji yao maalum.
Matokeo ya Tafiti kuondoa adha ya
wanawake watumia kuni
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano), Mhe. Stephen Masele.
Na Johary Kachwamba - MAELEZO, DODOMA
Matokeo ya Tafiti kuondoa adha ya
wanawake watumia kuni
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano), Mhe. Stephen Masele.
Na Johary Kachwamba - MAELEZO, DODOMA
TAFITI mbalimbali zimefanyika na zinaendelea kufanyika ili kupata majiko mbadala yasiyotumia nishati ya kuni hapa nchini.
Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano), Mhe. Stephen Masele wakati akijibu swali la msingi la Mhe. Amina Makilagi, Mbunge wa Viti Maalum iliyehoji matumizi ya tafiti za kupata majiko mbadala.
“Tafiti hizi zinahusu matumizi ya gesi inayotokana na kinyesi cha mifugo, matumizi ya gesi asilia, matumizi ya nishati itokanayo na mimea, matumizi ya makaa ya mawe, tungamotaka na majiko yanayotumia kiasi kidogo cha kuni na mkaa” alisema Mhe. Masele.
Alisema baadhi ya taasisi zinazofanya utafiti huu ni pamoja na Chuo Kikuu cha Dar-es-salaam, Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine, COSTECH, CARMATEC, MIGESADO na TaTEDO.
Mhe. Masele amesema Serikali imekuwa ikitumia matokeo ya tafiti hizi katika utekelezaji wa miradi ya hifadhi ya mazingira kama vile Mradi wa Hifadhi ya Mazingira wa Ziwa Tanganyika ambao umewezesha baadhi ya taasisi za Magereza, JKT, Shule za Sekondari na Vyuo vya Ualimu na Wananchi kutumia majiko hayo katika mikoa ya Katavi, Rukwa na Kigoma.
Aidha Serikali kupitia Mradi wa Kuhimili Mabadiliko ya Tabianchi katika maeneo ya Pwani unaotekelezwa katika mikoa ya Pwani na Dar-es-salaam kwa mwaka wa fedha 2014/2015 itasambaza majiko 1500 kwa kaya na kutoa mafunzo ya matumizi ya majiko hayo katika Wilaya za Ilala, Temeke na Kinondoni.
“napenda kuhimiza taasisi na wananchi kutumia majiko yanayotokana na tafiti hizi ili kupunguza matumizi makubwa ya kuni na mkaa, na pia kuondoa adha kwa wanawake ya kutafuta kuni, kupunguza athari kwa afya zao na pia kuchangia katika hifadhi ya Mazingira” alisisitiza Mhe. Masele.
Serikali kwa kushirikiana na taasisi binafsi imeendelea kusambaza technolojia hii na kutoa elimu ya matumizi ya majiko haya kupitia vyombo vya habari, maonyesho na maadhimisho ya na Siku ya Mazingira Duniani.
Spika atoa Ufafanuzi juu ya Muswada wa Binafsi wa
Mhe. John Mnyika
Spika wa Bunge la Tanzania Mhe. Anne Makinda
Na Anitha
Jonas-MAELEZO, Dodoma.
SPIKA wa Bunge la Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe. Anne Makinda ametoa ufafanuzi juu ya suala la Muswada binafsi
wa Baraza la Vijana uliyowasilishwa na Mhe. John
Mnyika Mbunge wa Ubungo (CHADEMA) hapo mwaka jana.
Mhe.Makinda alisema Ofisi yake
inataratibu zinazofuatwa katika uwasilishwaji wa Miswada bungeni na Kamati ya Bunge
ya Kudumu ya Maendeleo ya Jamii ilifanya taratibu zake na kuiletea Ofisi yake
taarifa ya makubaliano ya Muswada wa Serikali ndiyo utako somwa Bungeni baada
ya kufuata taratibu zote muhimu.
“Ofisi yangu haifanyi
maamuzi binafsi katika uwasilishwaji wa
Miswada Bungeni na zipo hatua mbalimbali Miswada inayopitia pamoja na Kanuni za Bunge zinatoa
muongozo katika utekelezaji wake na Kamati huzingatia hayo na mwisho hutoa taarifa ya kuomba Muswada kusomwa ndani ya Bunge,”alisema
Mhe.Makinda.
Naye Mwenyekiti wa Kamati ya
Kudumu ya Maendeleo ya Jamii Mhe.Said
Mtanda (Mb) wa Mchinga CCM alisema Kamati ilipokea Miswada miwili ya kuundwa
kwa Baraza la Vijana ukiwemo wa Mhe.John Mnyika Mb wa Ubungo CHADEMA na Muswada
wa Serikali.
Baada ya hapo Kamati ilikaa
Kikao tarehe 20-31 Oktoba 2014 na
kujadili Muswada huo ambapo pamoja na mambo mengine iliwaita wadau mbalimbali
ambao walitoa maoni yao na mapendekezo
ya Kamati,Kamati iliona Muswada huo haukuwa tayari na hivyo ulirudishwa katika
Ofisi ya Spika tarehe 06 Novemba,2014.
Aidha,Kamati ilipokea
Muswada wa Serikali kuhusu hoja ya kuanzishwa kwa Baraza la Vijana Tanzania
Muswada na Kamati ilipata nafasi ya kuujadili kwa kina, kupata maoni, ushauri na
mapendekezo ya wadau na hivyo badae kamati iliamua kuwa mtoa hoja Binafsi na Serikali
wakutane na na kushauriana kisha kupata muafaka wa Muswada upi uingie ndani ya
bunge.
“Kamati ilipata nafasi ya
kujadili hoja zote mbili na kufanya uamuzi wa kidemokrasia wa mashauriano na
maridhiano juu ya muswada upi uingie ndani ya Bunge.
Aidha Kamati ilizingatia
Kanuni ya 177 ya Kanuni za Kudumu za Bunge, inayosema akidi ya Mkutano wowote wa
Kamati ya kudumu itakuwa theluthi moja ya wajumbe wote wa kamati, kwenye kikao
hicho kulikuwa na wajumbe 13 kati ya 22 wa kamati nzima na hivyo theluthi moja
ya wajumbe hao ni 7, wajumbe 9 walipiga kura ya Muswada wa Serikali usomwe
bungeni wajumbe wanne wa walikataka Muswada binafsi uswomwe bungeni”,alisema
Mhe. Mtanda.
Mwisho Kamati ilikubali kwa
pamoja mambo yote ya msingi yaliyomo kwenye Muswada binafsi yatumike kuboresha
Muswada wa Serikali utakaowasilishwa Bungeni.
Waziri wa Nishati na
Madini (wapili kulia), Mhe. George Simbachawene akizungumza na waandishi wa
Habari Mjini Dodoma kuhusu Ugunduzi wa nane wa gesi asilia uliyofanywa na
Kampuni ya Statoil katika eneo la Bahari Kuu. Wa kwanza kulia ni Naibu Waziri
Nishati na Madini Dkt. Charles Mwijage na wa kwanza kushoto ni Mwenyekiti wa
Kamati ya Kudumu Nishati na Madini Mhe. Richard Ndassa (Mb) wa Sumve CCM. (Picha na Anitha Jonas – MAELEZO, Dodoma)
No comments:
Post a Comment