Kaimu Mkurugenzi Msaidizi Kitengo cha Tiba Asilia na Tiba Mbadala, Dk. Paulo Mhame, akizungumza na waandishi wa habari, Dar es Salaam leo kuhusu kazi na wajibu ya Wizara kwa jamii, Pia maendeleo ya masuala ya Tiba Asili na Tiba Mbadala nchini. Kulia ni Ofisa Habari wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Catherine Sungura. (Picha zote na Kassim Mbarouk-www.bayana.blogspot.com)
Msajili Baraza la Tiba Asili na Tiba Mbadala, Mboni Zuwena Bakari, akifafanua jambo kwa waandishi wa habari, wakati alipokuwa akielezea kuhusu maendeleo ya tiba hiyo. Katikati ni Kaimu Mkurugenzi Msaidizi Kitengo cha Tiba Asilia na Tiba Mbadala, Dk. Paulo Mhame na kulia ni Ofisa Habari wa Wizara, Catherine Sungura.
Kaimu Mkurugenzi Msaidizi Kitengo cha Tiba Asilia na Tiba Mbadala, Dk. Paulo Mhame, akizungumza na waandishi wa habari, Dar es Salaam leo kuhusu kazi na wajibu ya Wizara kwa jamii, Pia maendeleo ya masuala ya Tiba Asili na Tiba Mbadala nchini. Kushoto ni Msajili Baraza la Tiba Asili na Tiba Mbadala, Mboni Zuwena Bakari na kulia ni Ofisa Habari wa Wizara, Catherine Sungura.
Kaimu Mkurugenzi Msaidizi Kitengo cha Tiba Asilia na Tiba Mbadala, Dk. Paulo Mhame, akizungumza na waandishi wa habari, wakati wa mkutano huo, Dar es Salaam leo.
Baadhi ya waandishi wa habari, wakiwa kwenye mkutano huo jijini leo.
Ndugu
Waandishi wa Habari
Maendeleo ya tiba asili nchini
yalianza mara baada ya Uhuru. Aidha, nia halisi ya Serikali ya kuleta maendeleo
katika tiba asili ilijidhihirisha mwaka 1969 na kujifunua mwaka 1974 Julai, Serikali
ilipoanzisha kitengo cha utafiti katika tiba asili kwenye Kitivo cha Afya cha
Muhimbili. Leo hii kitengo kile kimekuwa Taasisi kamili chini ya Chuo Kikuu
kamili cha MUHAS.
Maendeleo ya jambo linalohusisha
taasisi zaidi ya moja huchukua muda mrefu, tiba asili vivyo hivyo. Hadi mwaka,
2002 Serikali ilitunga sheria Na. 23 ya
Tiba Asili na Tiba Mbadala. Katika kipindi hichohicho Taasisi ya Utafiti wa
Magonjwa ya Binadamu ilianzisha Idara ya utafiti wa tiba asili kwa lengo la
kuongeza nguvu za utafiti.
Mwaka 2005 BARAZA la kwanza la Tiba
Asili na Tiba Mbadala lilianzishwa kwa mujibu wa sheria Na. 23 ya mwaka 2002.
Baraza liliweka utaratibu wa namna ya kuwasajili waganga wa tiba asili na tiba
mbadala.
Waganga wa tiba mbadala ni wataalamu
wa tiba kulinga na tiba asili za nchi zisizo za Kiafrika kusini ya jangwa la
sahara. Taaluma hizo ni nyingi na zinahusisha nchi nyingi dunia; kwa mfano Tiba
Asili ya Kichina, Tiba Asili ya Korea, Tiba Asili ya India, Tiba Asili ya
Ugiriki, Ujerumani, Uingereza nakadhalika.
Waganga wa tiba asili wa asili ya
Tanzania pia wapo wa aina nyingi kulingana na kabila analotoka. Tanzania Bara
kuna aina 120 au zaidi za makabila na hivyo kuna taaluma za tiba asili 120.
Inakadiriwa kuwa Tanzania Bara ina waganga na wakunga wa tiba asili 75,000.
Idadi hii ni kubwa kuweza kuiratibu na kuwasajili kwa kupindi kifupi.
Pamoja na ugumu huo BARAZA limeweza kuwahamasisha na
kuwasajili waganga 6000 nchi nzima na bado kazi ya kuwasajili inaendelea.
Ili kurahisisha kazi ya uhamasishaji
na usajili kufanyika, Baraza kwa kushirikiana na Serikali wameteuliwa waratibu
wa tiba asili katika ngazi za mikoa na halmashauri.
Tunawashukuru sana waratibu hao kwa
kuitikia wito wa uteuzi wao huo kwani kazi iliyopo mbele yetu siyo nyepesi ina
changamoto nyingi. Moja ya changamoto zilizopo ni kuwa taaluma ya tiba asili ya
asili ya Tanzania haipo katika maandishi. Kinachozungumzwa siyo rahisi
kukithibitisha na hususan jambo lisilohusisha
dawa ambazo ndizo pekee zinafanyiwa utafiti na Taasisi zetu.
KUANZISHWA
KWA SHIRIKISHO LA VYAMA VYA WAGANGA WA TIBA ASILI TANZANIA
Katika kuweza kufanisha malengo ya
kuendeleza na kuboresha huduma za tiba asili nchini Serikali ilikaa na vyama
vya waganga wa tiba asili ili kuweza kuungana na kuunda Shirikisho la Vyama vya
Tiba Asili Tanzania (SHIVYATIATA). Baadhi ya malengo ya SHIVYATIATA ni kuviwakilisha vyama wanachama na kuwa msemaji mkuu
wa vyama vya Tiba Asili kwa Serikali, Taasisi za kitaifa, kimataifa na mahali
popote pale itakapotakiwa. Pili ni kuvishirikisha vyama wanachama wa Tiba Asili
nchini Tanzania kuungana kwa lengo la kuleta ushirikiano na mahusiano yenye
manufaa miongoni mwa vyama, wanachama, Serikali na mashirika mengine ya kitaifa
na kimataifa ili kuwa na mtizamo wa pamoja katika kuboresha taaluma, tafiti, haki
na maslahi yatokanayo na Tiba Asili. Tatu kuwafanya watabibu wa Tiba Asili
nchini wa shirikiane, wawe wamoja na kauli moja kwa ajili ya kulinda taaluma ya
Tiba Asili, kutetea kazi na maslahi yatokanayo na kazi ya Tiba Asili nchini
Vivyo hivyo kwa waganga wa tiba
mbadala nao wamaanzisha Chama cha Waganga wa Tiba Mbadala Tanzania.
CHANGAMOTO
ZA UENDELEZAJI NA UBORESHAJI WA TIBA ASILI TANZANIA
Pamoja kuwa mwaka huu tunafikia mwaka
wa 54 wa Uhuru wetu, katika kuboresha na kuendeleza huduma za Tiba Asili tuna
changamoto nyingi.
Ø
Moja
utafiti wetu haujatoa majibu yanayokusudiwa, ikiwa pamoja na kupata dawa zetu
za asili au zilizoboreshwa kutoka katika miti dawa yetu.
Ø
Utoaji
wa huduma katika tiba asili usiohusisha dawa hauna maelezo ya kisayansi
Ø
Waganga
na wakunga wa tiba asili waliopo ni wengi na ni changamoto ya kuwafikia wote
mara moja
Ø
Utoaji
wa huduma za tiba asili unatolewa kwa aina 120 tofauti
Ø
Waganga
au wakunga wa tiba asili wanazo taaluma za asili zaidi ya uganga au ukunga.
Kwa kuwa kabla ya miaka ya 1880 mtu
anayeitwa mganga walijumuisha:
Ø
Mganga
wa kutibu na kuponya
Ø
Mganga
wa kumshauri kiongozi kuhusu namna bora ya kutawala
Ø
Mganga
wa kumshauri kiongozi kuhusu namna bora ya kuleta ustawi katika eneo lao
Ø
Mganga
wa kumshauri kiongozi kuhusu kwenda au kutokwenda vitani na wahasimu wao
Leo makundi hayo yote hayapo lipo
kundi moja tu la waganga wa tiba asili, inakuwa siyo rahisi kumtambua yupi
mwenye taaluma nyingine pia.
Kuwa na aina nyingi za tiba asili
(120) na kuwepo kwa vyama vingi vya waganga wa tiba asili nayo ni changamoto
inayoathiri:
Ø
Ushirikishwaji
wa mganga ili kuboresha huduma za tiba asili
Ø
Vyama
kutumika kama chachu ya mganga kufanya kazi kwa pamoja kwa kuungana
Ø
waganga
wa taaluma tofauti kutofanya kazi kwa pamoja kiushirika kwa kuungana na kutoa
huduma au kuuza dawa zao
Ndugu
waandishi wa habari,
MATUMIZI
YA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU TIBA ASILI TANZANIA
Kupitia kazi yenu ya uandishi wa
habari ni matarajio makubwa ya BARAZA
na Serikali kuwa mtawahabarisha wananchi kuhusu tiba asili na tiba mbadala kwa
kuzingatia sheria, kanuni na miongozo iliyopo. Kwa kufanya hivyo wananchi
watapata taarifa zilizo sahihi.
Kuna taarifa za aina nyingi
zinazohusu tiba asili na tiba mbadala;
Ø
Uelimishaji hii ni kwa kuwa wananchi wengi hawajui kuhus
tiba asili na au tiba mbadala [taarifa hizi zitolewe na wataalamu waliobobea na
taarifa zenyewe ziwe zimehakikiwa na BARAZA
kama sheria inavyoelekeza]
Ø
Dawa
na matumizi ya dawa mbalimbali zinazotolewa [sheria inazuia kutangaza]
Ø
Kutangaza
kituo kinachotoa huduma za tiba asili na tiba mbadala [sheria inazuia kutangaza
vituo vinavyotoa huduma za tiba]
Ni matarajio ya Serikali na Baraza
kuwa vyombo vya habari vitajitahidi kufanya kazi kulingana na sheria, kanuni na
miongozo.
LOOK AT ME MY WEBSİTE TURKEY
ReplyDeletetravesti
travesti
travestitravesti
travesti
izmir travestileri
istanbul travestileri
ankara travestileri
mersin travestileri
bursa travestileri
izmir travestileri
konya travestileri
diyarbakır travestileri
mersin travestileri
sakarya travestileri
sakarya travestileri
istanbul travestileri
adana travestileri
antalya travestileri
eskisehir travestileri
samsun travestileri
kocaeli travestileri
izmir travestileri
eskisehir travestileri
kayseri travestileri
eskisehir travestileri
gaziantep travestileri
adana travestileri
samsun travestileri
izmir travestileri
eskisehir travestileri
travesti
kayseri travestileri
travesti
istanbul travestileri
istanbul travestileri
kocaeli travestileri
travesti
travesti
travesti