TANGAZO


Thursday, March 12, 2015

BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU YAZUNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI JIJINI DAR ES SALAAM NA KUTOA TAARIFA


Mkurugenzi Msaidizi wa Habari, Elimu na Mawasiliano wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu, Cosmas Mwaisobwa, akizungumza na waandishi wa habari, Dar es Salaam jana, kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu mikopo hiyo, yakiwemo masharti, urejeshaji pamoja na hatua zinazoweza kuchukuliwa kwa wahusika ambao hawajarejesha mikopo waliopatiwa na bodi hiyo. Kushoto ni Mkurugenzi wa Urejeshwaji Mikopo, Juma Chagonja. (Picha zote na Kassim Mbarouk-www.bayana.blogspot.com)
Mkurugenzi Msaidizi wa Habari, Elimu na Mawasiliano wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu, Cosmas Mwaisobwa, akizungumza na waandishi wa habari, Dar es Salaam jana, kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu mikopo hiyo. Kushoto ni Mkurugenzi wa Urejeshwaji Mikopo, Juma Chagonja na kulia ni Ofisa Habari Mwandamizi-Habari, Elimu na Mawasiliano wa bodi hiyo, Veneranda Malima.
Waandishi wa habari, wakimsikiliza Mkurugenzi Msaidizi wa Habari, Elimu na Mawasiliano wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu, Cosmas Mwaisobwa, alipokuwa akizungumza nao, kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu mikopo hiyo ya wanafunzi wa Elimu ya Juu jijini jana.
Wapigapicha wa vyombo mbalimbali vya habari, wakichukua matukio na maelezo yaliyokuwa yakitolewa na Mkurugenzi Msaidizi wa Habari, Elimu na Mawasiliano wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu, Cosmas Mwaisobwa, wakati wa mkutano huo jijini jana. 
Mkurugenzi Msaidizi wa Habari, Elimu na Mawasiliano wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu, Cosmas Mwaisobwa, akitoa ufafanuzi wakati alipokuwa akijibu maswali ya waandishi wa habari, wakati wa mkutano huo. Kushoto ni Mkurugenzi wa Urejeshwaji Mikopo, Juma Chagonja na kulia ni Ofisa Habari Mwandamizi-Habari, Elimu na Mawasiliano wa bodi hiyo, Veneranda Malima.
Mkurugenzi Msaidizi wa Habari, Elimu na Mawasiliano wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu, Cosmas Mwaisobwa, akijibu, maswali ya waandishi wa habari kwenye mkutano huo. Kushoto ni Mkurugenzi wa Urejeshwaji Mikopo, Juma Chagonja.

1.0        UTANGULIZI
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu ilipoanzishwa mwaka 2005 pamoja na utekelezaji wa Sera ya Uchangiaji, ilipewa majukumu mawili makubwa; kutoa mikopo kwa wanafunzi wahitaji na kurejesha mikopo kutoka kwa wanufaika wa mikopo hiyo ili kuufanya mfuko wa mikopo ya elimu kuwa endelevu.
Mikopo ya wanafunzi ilianza kutolewa mwaka 1994/1995 kupitia iliyokuwa  Wizara ya Elimu ya Juu, Sayansi na Teknolojia. Wakati huo serikali ilikuwa haikusanyi madeni kutoka kwa wanufaika hadi Bodi ilipoanza kufanya kazi.
Kampeni za urejeshaji mikopo zilianza rasmi mwaka 2006/2007, na tangu wakati huo kumekuwa na mafanikio makubwa katika ukusanyaji wa madeni kutoka kwa wanufaika wa mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu.

1.1        Mikopo iliyotolewa
Jumla ya Sh. 1,807,223,411,221.00 zimekopeshwa kwa wanafunzi kati mwaka wa masomo 1994/1995 na mwezi Juni, 2014.  Kati ya hizo, Sh. 51,103,685,914 zilitolewa na iliyokuwa Wizara ya Elimu ya Juu, Sayansi na Teknolojia na kiasi kilichobaki cha Sh. 1,756,119,725,307.00 kimetolewa na Bodi ya Mikopo tangu mwezi Julai, 2005 ilipoanza kazi rasmi.

1.2   Urejeshaji wa mikopo
Kiasi cha mikopo kilichokwishaiva na hivyo kuwa tayari kwa marejesho ni jumla ya Sh. 833,476,985,770.75 hadi kufikia tarehe 28 Februari, 2015.  Kati ya fedha hizo, mikupuo iliyokuwa tayari kurejeshwa ni kiasi cha Sh. 123,828,003,422.67. Kiasi cha mikopo kilichokuwa kimekusanywa kutoka kwenye mikopo iliyoiva ni Sh. 65,275,252,446.49 ambazo ni sawa na asilimia 53 ya mikupuo iliyokuwa tayari kurejeshwa hadi kufikia tarehe 28 Februari, 2015.
Aidha, jumla ya Wadaiwa 136,198 (sawa na asilimia 76.94 ya wadaiwa wote 177,017 ambao mikopo yao imeiva) wametambuliwa na wanaendelea na marejesho ya mikopo hadi tarehe 28 Februari, 2015.
Jedwali 1: Takwimu za Urejeshaji wa Mikopo ya Wanafunzi
Mwaka
Urejeshaji kwa mwaka (Tzs)
Jumla (Tzs)
2006/2007
53,616,011.22
53,616,011.22
2007/2008
858,941,262.29
912,557,273.51
2008/2009
1,176,404,180.00
2,088,961,453.51
2009/2010
2,147,075,264.78
4,236,036,718.29
2010/2011
4,409,171,729.99
8,645,208,448.28
2011/2012
11,508,714,785.96
20,153,923,234.24
2012/2013
14,850,247,552.21
35,004,170,785.45
2013/2014
18,088,801,344.43
53,092,972,129.88

1.3      Tozo la Utunzaji wa thamani ya mikopo
Hadi sasa, mikopo yote inayotolewa na Bodi kuanzia mwaka wa masomo 1994/1995 inabeba tozo la utunzaji wa thamani ya mikopo (value retention fee) kwa asilimia 6 kwa mwaka, kwa kiasi chote cha mkopo ambacho hakijarejeshwa.



2     MIKAKATI YA UREJESHAJI WA MIKOPO NA CHANGAMOTO ZILIZOPO

2.3        Mikakati ya Urejeshaji mikopo

Bodi inaendelea kuongeza kasi ya urejeshaji wa mikopo kwa kubuni mikakati kadhaa ikiwa ni pamoja na:
(i)               Kuendelea kutoa elimu kwa umma juu ya umuhimu wa kurejesha mikopo
(ii)              Kuongeza matumizi ya mitandao ya simu (M-pesa/Airtel Money) katika kukusanya madeni.
(iii)             Kuzidisha ushirikiano zaidi na wadau muhimu hasa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii, Mamlaka ya Mapato, Waajiri, Sekta isiyo rasmi na Wanufaika wa mikopo.
(iv)            Kuchukua hatua za kisheria dhidi ya Wanufaika wanaokaidi kurejesha mikopo yao. Hadi sasa kuna kesi 18 zilizofunguliwa mahakamani dhidi ya wadaiwa sugu.
(v)            Kutumia mfumo wa “LAWSON” katika kubaini Wadaiwa na kukusanya madeni kutoka   kwa Waajiriwa wa Serikali.
(vi)          Kushirikiana na Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Heasbu za Serikali katika kuhakiki uwajibikaji wa Waajiri katika kutekeleza wajibu wao katika urejeshaji wa mikopo.

2.2 Changamoto zilizopo na mikakati ya kukabiliana nazo
(i)          Imani potofu kwamba mikopo inayotolowa na Bodi ni ruzuku
Bado kuna baadhi ya Wadau wenye imani potofu kuwa fedha zitolewazo na Bodi ni ruzuku. Imani hii potofu inazorotesha juhudi za ukusanyaji wa madeni na inachangia ongezeko la waombaji wa Mikopo hata wale ambao wana uwezo wa kujigharamia.
         
Mkakati wa kukabiliana na changamoto hii ni kwa Bodi kuendelea kuelimisha umma na kuongeza jitihada za ukusanyaji madeni ili kusisitiza ujumbe kwamba hii ni mikopo ni si ruzuku.
(ii)        Kukosekana kwa ushirikiano wa kutosha kutoka kwa baadhi ya Wadau
Baadhi ya Wadau hasa waajiri na Wadaiwa hawawajibiki ipasavyo kwa mujibu wa Sheria katika kurejesha mikopo, kusaidia kuwatambua na kuwasilisha taarifa za wanufaika wa mikopo ya elimu ya juu.
Mkakati wa kukabiliana na changamoto hii ni kwa Bodi kuendelea kuwaelimisha waajiri na umma kwa ujumla kuhusu umuhimu wa kushirikiana na Bodi katika zoezi la kurejesha Mikopo.

2.4        Hitimisho

Kwa Taarifa hii, Bodi inawasisitizia wanufaika wa Mikopo, wazazi/walezi, waajiri na umma kwa ujumla kutambua kuwa Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu ni sehemu ya utekelezaji wa Sera ya Uchangiaji wa Elimu ya Juu. Hivyo ni muhimu kushirikiana katika kufanikisha marejesho ya mikopo iliyoiva ili kuuwezesha mfuko wa ukopeshaji kuwa endelevu na kutoa nafasi kwa wahitaji wengi zaidi kunufaika na mikopo ya elimu ya juu.
                  
Imetolewa na:
KITENGO CHA HABARI, ELIMU NA MAWASILIANO

BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU

No comments:

Post a Comment