TANGAZO


Saturday, January 3, 2015

Rais Dk. Shein azindua maegesho na njia za Ndege, Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Karume mjini Zanzibar

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa  Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein akisalimiana na Viongozi wakati alipowasili katika uzinduzi wa maegesho na njia ya kupitia Ndege (APRON AND TAXIWAY) leo  katika kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Abeid Amani Karume -Zanzibar huko Kiembesamaki nje ya Mji wa Unguja katika shamra shamra za kutimiza miaka 51 ya Mapinduzi matukufu ya Zanzibar. (Picha zote na Ikulu)
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa  Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein na Kaimu Meneja wa Benki ya Dunia Tanzania Monthe Biyoudi wakikata utepe kuzindua maegesho na njia ya kupitia Ndege (APRON AND TAXIWAY) leo katika kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Abeid Amani Karume -Zanzibar huko Kiembesamaki nje ya Mji wa Unguja katika shamra shamra za kutimiza miaka 51 ya Mapinduzi matukufu ya Zanzibar(kushoto0 Waziri wa Miundombinu na Mawasiliano Juma Duni Haji.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa  Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein na Kaimu Meneja wa Benki ya Dunia Tanzania Monthe Biyoudi wakifungua pazia kwa pamoja  kuzindua maegesho na njia ya kupitia Ndege (APRON AND TAXIWAY) leo katika kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Abeid Amani Karume -Zanzibar huko Kiembesamaki nje ya Mji wa Unguja katika shamra shamra za kutimiza miaka 51 ya Mapinduzi matukufu ya Zanzibar.
Wananchi na Viongozi mbali mbali walioalikwa katika sherehe za uzinduzi wa maegesho na njia ya kupitia Ndege (APRON AND TAXIWAY) leo katika kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Abeid Amani Karume -Zanzibar huko Kiembesamaki nje ya Mji wa Unguja katika shamra shamra za kutimiza miaka 51 ya Mapinduzi matukufu ya Zanzibar. 
Ndege zmbali mbali zikiwa katika Paki ikionesha  sura halisi ya uwanja wa Ndege wa Kimataifa cha Abeid Amani Karume -Zanzibar ilivyo ambapo  Ndege za mashirika mbali mbali ya ndege zinaouwezo wa kutua hapa nchini na kuweza kukuza pato la Taifa letu.
Msoma Risala Farida Rajab Yussuf akisoma risala hiyo mbele ya mgeni rasmi Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa  Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein wakati wa uzinduzi wa maegesho na njia ya kupitia Ndege (APRON AND TAXIWAY) leo  katika kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Abeid Amani Karume -Zanzibar huko Kiembesamaki nje ya Mji wa Unguja katika shamra shamra za kutimiza miaka 51 ya Mapinduzi matukufu ya Zanzibar.
Wasanii wa Ngoma ya Kibati wakitoa burudani yao wakati wa sherehe za uzinduzi wa maegesho na njia ya kupitia Ndege (APRON AND TAXIWAY) uzinduzi uliofanyika leo  katika kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Abeid Amani Karume -Zanzibar huko Kiembesamaki nje ya Mji wa Unguja ikiwa ni katika shamra shamra za kutimiza miaka 51 ya Mapinduzi matukufu ya Zanzibar ambapo Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa  Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein alikuwa mgeni rasmi wa shuhuli hiyo.
Waziri wa Miundombinu na Mawasiliano Juma Duni Haji akitoa nasaha fupi na kumkaribishaRais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa  Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein kutoa hutuba yake wakati wa uzinduzi wa maegesho na njia ya kupitia Ndege (APRON AND TAXIWAY) leo  katika kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Abeid Amani Karume -Zanzibar huko Kiembesamaki nje ya Mji wa Unguja katika shamra shamra za kutimiza miaka 51 ya Mapinduzi matukufu ya Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa  Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein akitoa hutuba yake wakati wa sherehe za uzinduzi wa maegesho na njia ya kupitia Ndege (APRON AND TAXIWAY) uzinduzi uliofanyika leo  katika kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Abeid Amani Karume -Zanzibar huko Kiembesamaki nje ya Mji wa Unguja ikiwa ni katika shamra shamra za kutimiza miaka 51 ya Mapinduzi matukufu ya Zanzibar.


Na Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein amezitaka taasisi za serikali na binafsi zinazofanya kazi katika uwanja wa ndege wa Abeid Amani Karume Zanzibar kuacha mivutano na badala yake washirikiane ili kuufanya uwanja huo kuwa ni kichocheo katika kukuza biashara na kuimarisha sekta ya utalii hapa nchini.

Dk. Shein aliyasema hayo leo huko Kisauni nje kidogo ya mji wa Zanzibar mara baada ya kuzindua maegesho na njia ya kupitia ndege katika kiwanja cha Kimataifa cha Abeid Amani Karume Zanzibar ikiwa ni miongoni mwa maadhimisho ya miaka 51 ya Mapinduzi ya Zanzibar ambapo viongozi mbali mbali na wananchi walihudhuria akiwemo Makamu wa Pili wa Rais Balozi Seif Ali Idd.
Katika maelezo yake Dk. Shein alisisitiza kuwa taasisi hizo ni lazima zikae pamoja na kushirikiana katika mambo na maamuzi yao kuamua wenyewe na si kupeleka Serikalini huku akiwataka kuanza taratibu hizo mapema kabla ya ujenzi wa jengo jipya la abiria hivi karibuni.

Aidha, Dk. Shein aliwataka watendaji na viongozi kufuata sheria na taratibu zilizowekwa na Serikali katika uwanja huo ikiwa ni pamoja na matumizi ya VIP na kuwataka viongozi kufuata sheria ya Mamlaka ya viwanja vya ndege iliyowekwa.

Alisema kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka hiyo tayari ameshapewa taratibu zote na tayari sheria ipo ambayo imepitishwa katika Baraza la Mapinduzi na kushangazwa na viongozi wanaowasakama wafanyakazi wa uwanja huo kwa kutofuata sheria na taratibu ziliopo.
“Tusirudishe nyuma taratibu zilizowekwa na Serikali katika uwanja wetu huu wa ndege na kila kiongozi anawajibu wa kufuata taratibu na sheria zilizopo sisi sote nadhani tunasafiri tunaenda Kusini, Kaskazini, Mashariki na Magharibi tunaona katika viwanja vya wenzetu wanavyokuwa makini... iweje sisi tuwe hivi”,alisema Dk. Shein kwa mshangao mkubwa.

Dk. Shein pia, alisisitiza kuwa suala la ulinzi na usalama ni la lazima katika viwanja vya ndege hivyo, ni lazima kuwepo ulizni wa uhakika katika uwanja huo ili kufuata sheria na taratibu za kimataifa za viwanja vya ndege ikiwa ni pamoja na kuwepo kwa huduama za zimamoto za uhakika.
 Pia, Dk. Shein alieleza azma ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kukijenga kiwanja cha ndege cha Pemba ndani ya mwaka huu ikiwa ni pamoja na kukiweka taa ili ndege ziweze kutua na kuruka wakati wa usiku ili uwanja huo uwe na hadhi inayokubalika.

Alisema kuwa tayari wameshajitokeza washirika wa maendeleo kutoka nchini Uturuki ambao wameonesha nia ya kukijenga kiwanja hicho cha ndege cha Pemba. Aidha, alieleza azma ya Serikali ya kujenga gati kubwa huko Mkoa wa Kaskazini Pemba ili kuepuka usumbufu wanaoupata wananchi wa Mkoa huo kwenda mkoa mwengine wa Kusini kufuata huduma hiyo.

Katika hotuba yake hiyo Dk. Shein alisikitishwa na kutokuwepo kwa takwimu za uhakika za uingiaji wageni katika uwanja huo wa ndege na kushangazwa na mamlaka zilizopo katika kiwanja hicho kwa kuchelea kutoa takwimu sahihi hali ambayo alisema inapelekea kuzorota kwa maendeleo hasa katika sekta ya utalii ambayo ndio nguzo kubwa ya uchumi wa Zanzibar.

Alionesha kushangazwa huko kwa kuwa utaratibu tayari umeshawekwa na kuzitaka taasisi zilizomo ndani ya uwanja huo kushirikiana kwa pamoja na kuacha mivutano kwani mivutano haijengi na badala yake inabomoa.

Alisema kuwa licha ya uhaba wa eneo liliopo ndani ya uwanja huo lakini haja ya kufanya kazi kwa kushirikiana ni muhimu kwani serikali baada ya kuliona tatizo hilo la uhaba wa eneo ndipo ilipolazimika kujenga jengo jipya la abiria.

Dk. Shein alisisitiza haja ya kuyaita mashirika ya ndege kuzileta ndege zao hapa Zanzibar kutokana na upanuzi huo wa uwanja wa ndege ikiwa ni pamoja na kukamilika kwa jengo jipya la abiria katika kiwanja hicho cha ndege cha Abeid Amani Karume

Alisema kuwa lengo kubwa ni kuirejesha Zanzibar kuwa kituo kikubwa cha kibiashara kama ilivyokuwa hapo siku za nyuma mnamo karne ya 19 na 20 ambapo Zanzibar iliweza kufanya biashara na Hongkong, Machester na sehemu nyenginezo.

Alisisitiza kuwa mbali ya malengo na jitihada hizo, pia Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ndani ya mwaka huu inakusudia kuingiza watalii laki5 kwani ujenzi wa huduma hizo za kiwanja cha ndege ni miongoni mwa vichocheo vikuu vya maendeleo.

Dk. Shein pia amezitaka taaisi zinazofanya kazi ndani ya uwanja huo wa ndege wa Kimataifa wa Zanzibar ziweze kubuni mambo mbali mbali na kuwa chanzo cha kushajiisha maendeleo yao  katika uwanja huo.
Aidha, Dk. Shein aliipongeza Kamati ya watu saba iliyokuwa ikiongozwa na Marehemu mzee Juma Ame ambayo imefanya kazi kubwa katika kuwatuliza wananchi wa eneo hilo la uwanja wa ndege baada ya kutokea mtafaruku mkubwa wakati wa ujenai huo ambapo wananchi hao walitakiwa nyumba zao kuvunjwa.

Naye Waziri wa Miundombinu na Mawasiliano Mhe. Juma Duni Haji alisema kuwa mafanikio makubwa yameweza kupatikana katika ujenzi huo na kueleza azma ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika ujenzi huo.

Aidha, Waziri huyo alitumia fursa hiyo kueleza changamoto zilizopo na juhudi za ufumbuzi zinazochukuliwa  huku akieleza kuwa tayari mashirika makubwa yameshaanza safari zake hapa Zanzibar na kueleza matarajio ya mashirika mengine makubwa duniani yakiwemo Qatar, Emirate, Fly Dubai, Turkish na mengineyo.
Mwakilishi wa Benki ya Dunia, Monthe Biyoundi nae alieleza kufarajika na hatua hiyo ya ujenzi iliyokamilika katika uwanja huo wa ndege wa Zanzibar na kusisitiza azma ya Benki hiyo ya kuendelea kuiunga mkono Zanzibar.

Mapema Katibu Mkuu wa Wizara ya Miundombinu na Mawasiliano Dk. Juma Malick Wakili akitoa maelezo ya kitaalamu alisema kuwa mkataba wa ujenzi huo ulitiwa saini baina ya Wizara ya Miundombinu na Mawasiliano na Kampuni ya SOGEA SATOM ya Ufaransa mnamo tarehe 18 Mei 2012 kwa gharama za Tsh. Bilioni 65.6.
Alisema kuwa mradi huo ulitarajiwa kuanza rasmi tarehe 02Julai 2012 baada ya utiaji saini, lakini kutokana na sababu mbali mbali za kiufundi mkandarasi alianza ujenzi Novemba 29, 2012 na kukamilika rasmi baada ya siku 740 yaani tarehe Disemba 9, 2014.

Alisema kuwa baada ya kukamilika kwa Mradi huo Kiwanja hicho kitakuwa na njia sita za kupitia ndege kuelekea na kutoka katika barabara ya kurukia na kutulia ndege zenye urefu wa mita 3,427 na upana wa mita 25 na mabega yenye upanda wa mita 9.5 kila upande.
Sambamba na hayo, Katibu Mkuu hyo alisema kuwa Serikali ya Mapindyuzi Zanzibar ilitumia jumla ya Tsh. Bilioni 1.2 kwa ajili ya kuwalipa fidia wananchi waliokua wakitumia eneo la mradi kama makaazi na amshamba yao pamoja na fidia ya kuhamisha makaburi 21 yaliokuwemo katika eneo hilo.

No comments:

Post a Comment