TANGAZO


Saturday, December 13, 2014

Waziri wa Mambo ya Ndani awaambia madereva chonde chonde zingatieni sheria za usalama barabarani

*Azindua rasmi kampeni ya “Wait to Send” ya Vodacom
Waziri wa Mambo ya Ndani  Mh.Mathias Chikawe (watatu kutoka kulia) akikata utepe kuashiria uzinduzi wa kampeni ya usalama barabarani uliofanyika eneo la Mwenge makutano ya barabara ya Sam Nujoma na Ali Hassan Mwinyi jijini  Dar es Salaam, uzinduzi huo uliambatana na  upimaji wa kiwango cha pombe mwilini kwa madereva na ugawaji wa pete maalumu za kuwakumbusha madereva kuacha kutumia simu za mkononi wanapokuwa wanaendesha vyombo vya moto,wanaoshuhudia ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Umma wa Vodacom Tanzania Rosalynn Mworia, Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Tanzania, Kamanda Mohammed Mpinga,mwenyekiti wa usalama barabarani wilaya ya Kinondoni Hua Tluway,wapili (kushoto) na Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani Hamza Kassongo na Henry  Bantu.
Waziri wa Mambo ya Ndani  Mh.Mathias Chikawe (watatu kutoka kulia) akikata utepe kuashiria uzinduzi wa kampeni ya usalama barabarani uliofanyika eneo la Mwenge makutano ya barabara ya Sam Nujoma na Ali Hassan Mwinyi jijini  Dar es Salaam, uzinduzi huo uliambatana na  upimaji wa kiwango cha pombe mwilini kwa madereva na ugawaji wa pete maalumu za kuwakumbusha madereva kuacha kutumia simu za mkononi wanapokuwa wanaendesha vyombo vya moto,wanaoshuhudia ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Umma wa Vodacom Tanzania Rosalynn Mworia, Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Tanzania, Kamanda Mohammed Mpinga,mwenyekiti wa usalama barabarani wilaya ya Kinondoni Hua Tluway,wapili (kushoto) na Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani Hamza Kassongo na Henry  Bantu.
Waziri wa Mambo ya Ndani  Mh.Mathias Chikawe (wapili kutoka kulia) Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Umma wa Vodacom Tanzania Rosalynn Mworia, Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Tanzania, Kamanda Mohammed Mpinga,mwenyekiti wa usalama barabarani wilaya ya Kinondoni Hua Tluway (wapili kushoto) na Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani Hamza Kassongo na Henry  Bantu (kulia) wakishangilia baada ya uzinduzi wa kampeni ya usalama barabarani uliofanyika eneo la Mwenge makutano ya barabara ya Sam Nujoma na Ali Hassan Mwinyi jijini  Dar es Salaam, uzinduzi huo uliambatana na  upimaji wa kiwango cha pombe mwilini kwa madereva na ugawaji wa pete maalumu za kuwakumbusha madereva kuacha kutumia simu za mkononi wanapokuwa wanaendesha vyombo vya moto.
Waziri wa Mambo ya Ndani  Mh.Mathias Chikawe akimsikiliza kwa makini Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Umma wa Vodacom Tanzania Rosalynn Mworia, wakati alipokuwa akimuelezea matumizi ya pete maalumu za kidoleni ambazo huwakumbusha madereva kuacha kutumia simu za mkononi wanapokuwa wanaendesha vyombo vya moto wakati wa uzinduzi wa kampeni ya usalama barabarani uliofanyika eneo la Mwenge makutano ya barabara ya Sam Nujoma na Ali Hassan Mwinyi jijini  Dar es Salaam, uzinduzi huo uliambatana na upimaji wa kiwango cha pombe mwilini kwa madereva Kushoto ni Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Tanzania, Kamanda Mohammed Mpinga Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani Hamza Kassongo na Henry M. Bantu (kulia)  na  Mjumbe wa  baraza hilo Hamza Kasongo.
Waziri wa Mambo ya Ndani  Mh.Mathias Chikawe akimsikiliza kwa makini Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Umma wa Vodacom Tanzania Rosalynn Mworia, wakati alipokuwa akimuelezea matumizi ya pete maalumu za kidoleni ambazo huwakumbusha madereva kuacha kutumia simu za mkononi wanapokuwa wanaendesha vyombo vya moto wakati wa uzinduzi wa kampeni ya usalama barabarani uliofanyika eneo la Mwenge makutano ya barabara ya Sam Nujoma na Ali Hassan Mwinyi jijini  Dar es Salaam, uzinduzi huo uliambatana na upimaji wa kiwango cha pombe mwilini kwa madereva Kushoto ni Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Tanzania, Kamanda Mohammed Mpinga Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani Hamza Kassongo na Henry M. Bantu (kulia)  na  Mjumbe wa  baraza hilo Hamza Kasongo.
Waziri wa Mambo ya Ndani  Mh.Mathias Chikawe (kushoto)  akimuonyesha  dereva wa pikipiki  pete zenye ujumbe wa “Wait to Send” wakati wa uzinduzi wa kampeni ya usalama barabarani uliofanyika eneo la Mwenge makutano ya barabara ya Sam Nujoma na Ali Hassan Mwinyi jijini  Dar es Salaam, uzinduzi huo uliambatana na  upimaji wa kiwango cha pombe mwilini kwa madereva na ugawaji wa pete maalumu za kuwakumbusha madereva kuacha kutumia simu za mkononi wanapokuwa wanaendesha vyombo vya moto.wengine wanaoshuhudia ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Umma wa Vodacom Tanzania Rosalynn Mworia na Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Tanzania, Kamanda Mohammed Mpinga
Waziri wa Mambo ya Ndani  Mh. Mathias Chikawe (kushoto)  akimvalisha dereva wa pikipiki  pete zenye ujumbe wa “Wait to Send” wakati wa uzinduzi wa kampeni ya usalama barabarani uliofanyika eneo la Mwenge makutano ya barabara ya Sam Nujoma na Ali Hassan Mwinyi jijini  Dar es Salaam, uzinduzi huo uliambatana na  upimaji wa kiwango cha pombe mwilini kwa madereva na ugawaji wa pete maalumu za kuwakumbusha madereva kuacha kutumia simu za mkononi wanapokuwa wanaendesha vyombo vya moto.wengine wanaoshuhudia ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Umma wa Vodacom Tanzania Rosalynn Mworia na Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Tanzania, Kamanda Mohammed Mpinga
Waziri wa Mambo ya Ndani  Mh. Mathias Chikawe (kushoto), akishuhudia  dereva wa pikipiki  akipimwa kilevi, wakati  wa  uzinduzi wa kampeni ya usalama barabarani uliofanyika eneo la Mwenge makutano ya barabara ya Sam Nujoma na Ali Hassan Mwinyi jijini  Dar es Salaam, uzinduzi huo uliambatana na  upimaji wa kiwango cha pombe mwilini kwa madereva na ugawaji wa pete maalumu za kuwakumbusha madereva kuacha kutumia simu za mkononi wanapokuwa wanaendesha vyombo vya moto.wengine wanaoshuhudia ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Umma wa Vodacom Tanzania Rosalynn Mworia na Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Tanzania, Kamanda Mohammed Mpinga.
Waziri wa Mambo ya Ndani  Mh. Mathias Chikawe (kushoto), akishuhudia  dereva wa daladala  akipimwa kilevi, wakati  wa  uzinduzi wa kampeni ya usalama barabarani uliofanyika eneo la Mwenge makutano ya barabara ya Sam Nujoma na Ali Hassan Mwinyi jijini  Dar es Salaam, uzinduzi huo uliambatana na  upimaji wa kiwango cha pombe mwilini kwa madereva na ugawaji wa pete maalumu za kuwakumbusha madereva kuacha kutumia simu za mkononi wanapokuwa wanaendesha vyombo vya moto.wengine wanaoshuhudia ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Umma wa Vodacom Tanzania Rosalynn Mworia na Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Tanzania, Kamanda Mohammed Mpinga.
Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Tanzania, Kamanda Mohammed Mpinga akijadiliana jambo na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Umma wa Vodacom Tanzania Rosalynn Mworia wakati wa uzinduzi wa kampeni ya usalama barabarani iliyozindiliwa  na Waziri wa Mambo ya Ndani  Mh. Mathias Chikawe katika eneo la Mwenge makutano ya Barabara ya Sam Nujoma na Ali Hassan Mwinyi jijini  Dar es Salaam leo, uzinduzi huo uliambatana na  upimaji wa kiwango cha pombe mwilini kwa madereva na ugawaji wa pete maalumu za kuwakumbusha madereva kuacha kutumia simu za mkononi wanapokuwa wanaendesha vyombo vya moto.

Madereva nchini wametakiwa kuzingatia sheria za barabarani,kutotumia vinywaji vyenye ulevi na kuacha tabia ya kuongea na simu au kutuma na kupokea ujumbe wa maneno (sms) wanapokuwa wanaendesha vyombo vya moto.
Wito huo umetolewa na Waziri wa Mambo ya Ndani,Mheshimiwa Mathias Chikawe, katika  kampeni ya uhamasishaji wa usalama barabarani iliyozinduliwa leo na serikali kupitia Jeshi la polisi,Baraza la Taifa la Usalama barabarani na kampuni ya mawasiliano ya Vodacom Tanzania eneo la Mwenge jijini Dar es Salaam ambapo pia alishiriki katika zoezi la  kuwagawia madereva pete maalum za kuwakumbusha kutotumia simu za  mkononi wanapokuwa wanaendesha magari na pikipiki.
Alisema madereva wakizingatia sheria za barabarani  kwa kiasi kikubwa ajali zinazoendelea kutokea kila siku zitapungua hususani katika kipindi hiki kuelekea sikukuu ya Krismas na mwaka mpya na aliipongeza Vodacom Tanzania kwa kuunga mkono jitihada za serikali katika kupambana na tatizo hili ambalo limekuwa sugu .
Naye  Mkuu wa kikosi cha usalama barabarani  cha Jeshi la Polisi, Kamanda Mohamed Mpinga amesema kampeni hii ni muhimu katika kupunguza matukio ya ajali “Watumiaji wa barabara  hususani madereva wa vyombo vya moto hawana budi kuzingatia maelekezo ambayo tumekuwa tukiwapa katika kampeni hizi ili tupate matokeo mazuri kwa kupunguza ajali kama ilivyokusudiwa”Alisema.
Kwa upande wake,Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano na uhusiano wa Umma  wa Vodacom,Rosalynn Mworia, alisema Vodacom itaendelea  kushirikiana na serikali kuunga mkono jitihada za kuondoa  matatizo kwenye jamii kama lilivyo tatizo hili la ajali ili kuhakikisha wananchi wanaishi maisha murua na marefu.”Tunaomba madereva kufuata sheria za barabarani kwa usalama wenu,usalama wa abiria mnaowabeba na watumiaji wengine wa barabara".
 Aliongeza kuwa Vodacom itakuwa mstari wa mbele kuelimisha jamii athari za kuendesha gari wakati huo huo unatumia simu  ya mkononi  kupitia kampeni  ya "Wait to Send" pia itaendelea kuhamasisha madereva kuzingatia sheria za usalama barabarani.Mbali na kampeni  hii alisema kwa mwaka huu kampuni ilidhamini Wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani.
Alisema kabla ya uzinduzi wa kampeni ya leo tayari umefanyika uhamasishaji wa madereva kuzingatia sheria za barabarani katika miji ya Dar es Salaam,Mwanza na kampeni itaendelea kufanyika sehemu mbalimbali nchini.
Katika uzinduzi huu wafanyakazi wa Vodacom kwa kushirikiana na askari wa  usalama barabarani walitoa uhamasishaji wa madereva kuacha kuongea na simu wanapoendesha vyombo vya moto pia zoezi la kupima madereva kubaini kama wanatumia vilevi lilifanyika.

No comments:

Post a Comment