TANGAZO


Wednesday, December 24, 2014

Kikundi cha Ngara Youth Foundation Chaishukuru Serikali kwa kupatiwa mkopo kutoka Mfuko wa Maendeleo ya Vijana

Mkurugenzi Msaidizi wa Ufuatiliaji na Tathimini  wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi. Verdiana Mushi akikagua mradi wa kikundi cha vijana kutoka Ngara alipowatembelea kwa ajili ya kutathmini maendeleo ya mfuko wa maendeleo wa vijana. Kulia ni Mwenyekiti  wa kikundi cha vijana cha Hekima Group Ngara  Bw.George  Kessy.

Katibu wa Ngara Saccoss Bw.Joackim  Jordan (wapili kushoto)  akiwaonesha Maofisa wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo walipowatembelea hivi karibuni baadhi ya tofali aina ya vibrated blocks zinazotengenezwa kwa udongo na simenti ambazo vikundi kumi vya vijana vilipata mafunzo ya kutengeneza matofali hayo kama sehemu ya  miradi wanayofanya. Kulia ni Mwenyekiti wa kikundi cha vijana cha Hekima Group Ngara  Bw. George  Kessy. (Picha zote na Anitha Jonas – Maelezo)




Na Anitha Jonas – Maelezo
KIKUNDI cha vijana  cha Ngara Youth Foundation chenye  wanachama  wapatao kumi  na moja  waliomaliza  elimu ya juu wamenufaika  baada ya kupata  mkopo wa Milioni tano  kupitia mfuko  wa Maendeleo ya Vijana na kuanzisha miradi miwili ikiwemo mradi wa kuuza mbao na  mradi wa kuosha magari.

Hayo yalisemwa  jana na  Katibu  wa kikundi hicho Bw. Jason  Athanas alipotembelewa na  maafisa kutoka  Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kutathimini  miradi inayoendeshwa na  vikundi  baada ya kupatiwa mkopo kwa ajili ya kujikwamua kiuchumi  kutokana na changamoto ya ajira iliyopo nchini.
Kikundi hicho kimeishukuru Serikali kwa kuwapatia  mkopo uliopelekea kuongeza kipato  kwa kila mwanachama hivyo kuboresha hali  ya maisha  baada ya kukosa ajira na kuwafanya kuwa wabunifu katika jamii.
“Tuliamua kuanzisha kikundi hiki baada ya kumaliza chuo na kutafuta ajira kwa muda mrefu hivyo tuliamuamu kuungana kuanzisha kikundi chetu ambapo tulibuni mradi tulioona unafaa na kuomba  mkopo, kwa sasa tuna miradi miwili ambayo ni mradi wa kuuza mbao na wakuosha magari (Car Wash)”,alisema Bw. Athanas.
Naye Mkurugenzi  Msaidizi  Tathmini na Ufuatiliaji kutoka  Wizara ya Habari, Vjana, Utamaduni na  Michezo Bibi.Verdiana Mushi, aliwapongeza vijana hao kwa juhudi kubwa wanazozifanya na kutoa wito kwa vijana  wengine kuiga mfano wa vijana hao kwa kuanzisha vikundi vyao na kuomba mkopo katika mfuko wa maendeleo ya vijana unaosimamiwa na Wizara.

Aidha  Ofisa  Vijana  kutoka  Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni  na  Michezo  Bw. Eliakim Mtawa aliwashauri vijana wa Ngara Youth Foundation kuendelea  kufanya kazi kwa bidii na kwa ubunifu huku wakizingati matumizi mazuri ya mapato yanayotokana na miradi yao pamoja na kuendelea kutafuta vyanzo mbalimbali  vya fedha kukua kiuchumi na kukuza miradi ya kikundi.

No comments:

Post a Comment