TANGAZO


Monday, September 1, 2014

Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba, Mhe. Samuel Sitta awaahidi walemavu kutendewa haki katika Katiba mpya ijayo


Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba, Mhe. Samuel Sitta akizungumza na watu wenye ulemavu wakati walipofika kuonana naye leo, Septemba 1, 2014 kwenye Ukumbi wa Pius Msekwa mjini Dodoma, kuhusu maoni yao katika Katiba Mpya ijayo. Mhe. Sitta aliwahakikishia suala la haki kwa watu wenye ulemavu kuzingatiwa katika Katiba Mpya ijayo.


Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba, Mhe. Samuel Sitta akiwahakikishia suala la haki kwa Watu wenye Ulemavu katika Katiba Mpya ijayo wakati wa mkutano na Shirikisho la Vyama vya Watu wenye Ulemavu (SHIVYAWATA) iliyofanyika 01 Septemba, 2014 kwenye Ukumbi wa Pius Msekwa mjini Dodoma.


Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Inclusive Development Promoters and Consultants ya Dar es Salaam, Bw. Kaganzi Rutachwamagyo akisoma taarifa ya hoja zao walizoziwasilisha mbele ya Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba wakati wa mkutano na Shirikisho la Vyama vya Watu wenye Ulemavu (SHIVYAWATA) iliyofanyika 01 Septemba, 2014 kwenye Ukumbi wa Pius Msekwa mjini Dodoma.


Baadhi ya wanachama wa Shirikisho la Vyama vya Watu wenye Ulemavu (SHIVYAWATA) wakifuatilia mada katika mkutano hiyo iliyofanyika 01 Septemba, 2014 kwenye Ukumbi wa Pius Msekwa mjini Dodoma.


Baadhi ya wanachama wa Shirikisho la Vyama vya Watu wenye Ulemavu (SHIVYAWATA) wakifuatilia mada katika mkutano hiyo iliyofanyika 01 Septemba, 2014 kwenye Ukumbi wa Pius Msekwa mjini Dodoma.



Baadhi ya Waandishi wa Habari wakifutilia mada ya mkutano hiyo iliyofanyika 01 Septemba, 2014 kwenye Ukumbi wa Pius Msekwa mjini Dodoma.


Baadhi ya Waandishi wa Habari wakifutilia mada ya mkutano hiyo iliyofanyika 01 Septemba, 2014 kwenye Ukumbi wa Pius Msekwa mjini Dodoma.



Katibu wa Shirikisho la Vyama vya Watu wenye Ulemavu (SHIVYAWATA) Bw. Felician Mkude (kushoto) akikabidhi taarifa kwa Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba, Mhe. Samuel Sitta wakati wa mkutano iliyofanyika 01 Septemba, 2014 kwenye Ukumbi wa Pius Msekwa mjini Dodoma.


Katibu wa Shirikisho la Vyama vya Watu wenye Ulemavu (SHIVYAWATA) Bw. Felician Mkude (kushoto) akikabidhi taarifa kwa Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba, Mhe. Samuel Sitta wakati wa mkutano iliyofanyika 01 Septemba, 2014 kwenye Ukumbi wa Pius Msekwa mjini Dodoma



Makamu Mwenyekiti wa Shirikisho la Vyama vya Watu wenye Ulemavu (SHIVYAWATA), Bi. Amina Mollel akichangia mada wakati wa mkutano iliyofanyika 01 Septemba, 2014 kwenye Ukumbi wa Pius Msekwa mjini Dodoma. (Picha zote na Benedict Liwenga, Maelezo-Dodoma)




Na Benedict Liwenga, Maelezo-Dodoma

01/09/2014.

MWENYEKITI wa Bunge Maalum la Katiba, Mhe. Samuel Sitta amewahakikishia watu wenye ulemavu nchini kuwa wanatendewa haki katika Katiba Mpya itakayopatikana.


Mhe. Sitta ameyasema hayo leo Septemba Mosi, 2014 katika mkutano wake na baadhi ya viongozi wa Shirikisho la Vyama vya Watu wenye Ulemavu Tanzania (SHIVYAWATA) ambalo lilikuja katika Bunge Maalum kwa lengo la kuwasilisha hoja zenye msisitizo kuhusu haki za watu wenye ulemavu katika mchakato Katiba Mpya.

Mhe. Sitta amesema kuwa kazi wanayoifanya ya kuyapokea makundi mbalimbali Bungeni hapo haina lengo la kuja na hoja mpya  na kuziwasilisha katika Bunge hilo, bali ni mawasiliano ya kawaida yanayohusu safari kutoka Rasimu Mpya ya Katiba mpaka kufikia katika Katiba Mpya inayopendekezwa ipatikane.


“Jambo lolote lililoandikwa na binadamu halikosi kasoro, katika Rasimu hii ya Katiba tumegundua inayomapungufu kadha wa kadha, kuna baadhi ya maoni ambayo hayakuzingatiwa ndiyo maana tunayafanyia kazi ili yawemo katika Katiba Mpya itakayopatikana,”.alisema Mhe. Sitta.


Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Inclusive Development Promoters and Consultants kutoka  Dar es Salaam, Bw. Kaganzi Rutachwamagyo ambaye pia ni mwanachama wa Shirikisho hilo,amesema kuwa Kikosi cha Ushauri kuhusu masuala ya watu wenye Ulemavu kimeweka kipaumbele cha msisitizo wao ambao unajielekeza katika hoja za kuongeza masuala ya mambo ya Muungano ambapo wamependekeza kuwa kwenye orodha ya Mambo ya Muungano kuongezewe suala moja zaidi la Nane kwa mujibu wa Rasimu ya Pili ya Katiba ambalo ni uratibu wa masuala ya haki, usawa na fursa na uwajibikaji kwa watu wenye ulemavu kama jambo la Muungano.

Bw. Rutachwamagyo  ameongeza kuwa hoja nyingine ya msisitizo inahusiana na suala la uanzishwaji wa chombo cha uratibu wa haki, usawa wa fursa na uwajibikaji wa haki za watu wenye ulemavu ambayo hii ni kwa mujibu wa Ibara ya 33 ya Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Watu wenye Ulemavu na Mkataba mwenza wa nyongeza iliyoridhiwa kwa pamoja na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na amesema kuwa wanataka chombo hiko kijulikane kama Tume ya Kitaifa Juu ya Haki, Usawa wa Fursa na Uwajibikaji kwa Watu wenye Ulemavu.


Aidha, Bw. Rutachwamagyo  amegusia pia juu ya hoja nyingine inayohusu suala la Uwakilishi wa watu wenye ulemavu kwenye Bunge la Tanzania, Baraza la Wawakilishi, Mabaraza ya Madiwani utamkwe na Katiba na ukokotolewe kwa misingi ya asilimia badala ya kuweka idadi mahsusi.


“Mathalani, tunapendekeza kifungu 113 kisomeke kuwa asilimia 5% ya Wabunge wote wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania watakuwa ni watu wenye ulemavu wakiwakilisha kundi hili na watapatikana kwa kuchaguliwa na wahusika wenyewe,” alisema .

Aliongeza kuongeza kwa kuzitaja hoja nyingine ikiwemo suala la matumizi ya lugha sanifu kwa muktadha wa watu wenye ulemavu na amesema kuwa kuna hali ya matumizi ya misamiati na islahi ambazo zinakinzana na dhana za walemavu kimataifa hivyo ni vema kukawa na tafsiri sahihi ya majina kwa watu hao ili kuepuka kukinzana huko, aidha amegusia pia suala la Hifadhi ya jamii huku akifafanua kuwa wadau wenye ulemavu nchini wanadai kuwepo kwa ibara maalum ndani ya Katiba inayoelekeza masharti ya upatikanaji wa hifadhi ya jamii kwa watu wenye Ulemavu ikiwa ni pamoja na kulipwa gharama ama kupewa unafuu ya kupunguza makali ya walemavu kwa mujibu wa ibara ya 28 ya Mkataba wa Haki za Watu wenye Ulemavu ya 2006.


Akiongea kwa niaba ya watu wenye ulemavu, Mhe. Amon Mpanjo ambaye ni mjumbe wa Bunge hilo amemuomba Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba kuunga mkono sio kupokea maoni mapya, bali kuyaboresha yale yaliyokwisha wasilishwa hapo awali.

“Tukuombe Mwenyekiti ulisisitizie Bunge letu Maalum la Katiba liweze kuzingatia haki za watu wenye Ulemavu ili nao wapate kuwa na maisha bora,” alisema Mpanjo.


Naye Makamu Mwenyekiti wa SHIVYAWATA, Bi. Amina Mollel amesisitiza juu ya hitaji la wanawake la hamsini kwa hamsini na kati ya hizo, asilimia 5% wawe ni wabunge walemavu na ameitaka Tanzania kuwa mfano wa kuigwa kwa kutoa nafasi nyingi za uongozi  kada mbalimbali kwa walemavu.


“Hii iwe chachu katika kuhakikisha kuwa watu wenye ulemavu wanapewa nafasi kwa uwezo walionao na sio kubaguliwa,” alisema Amina.

No comments:

Post a Comment