TANGAZO


Friday, August 1, 2014

Serikali yaunga mkono jitihada za wadau wa Michezo

Balozi wa Hispania nchini Tanzania Mh.  Luis Manuel  Ceuesta Civis  (Kulia) akiongea na Makocha kutoka Timu ya Barcelona ya nchini Hispania katika mkutano wa Wanahabari uliofanyika jijini Dar es Salaam jana (leo), makocha hao wapo nchini kwa ajili ya kutoa mafunzo ya siku mbili kwa makocha wazalendo, wa kwanza kushoto ni Kocha Daniel Bigas Alsina  na katikati ni Kocha Isaac Oriol Guerrero Hernandes.
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Vijana kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bi Juliana Yassoda (Katikati) akiongea na Wanahabari (Hawapo pichani) kuhusu makocha wa Timu ya Barcelona  kutoka nchini Hispania  ambao wako nchini kwa ajili ya  mafunzo ya makocha yatakayofanyika kwa muda wa siku mbili, wa kwanza kulia ni Balozi wa Spain nchini Mh. Luis Manuel Ceuesta Civis, mafunzo hayo yanatolewa kwa ushirikiano na Kiwanda cha Bia cha Tanzania Breweries.
Kocha Isaac Oriol Guerrero Hernandes (katikati)   kutoka timu ya Barcelona ya nchini Hispania (katikati) akitoa maelezo kwa wanahabari (hawapo pichani) kuhusu mafunzo ya siku mbili watakayotoa kwa makocha 30 wakizalendo, kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Vijana Bi. Juliana Yassoda na wa kwanza kushoto ni kocha Kocha Daniel Bigas Alsina. 
Makocha wa Kizalendo 30 ambao wanatarajiwa kupewa mafunzo ya siku mbili kutoka kwa makocha wa Barcelona wakiwa katika picha ya pamoja. (Picha zote na Benjamin Sawe kutoka Kitengo cha Mawasiliano Serikalini WHVUM)


Na Genofeva Matemu – Afisa Mawasiliano Serikalini, WHVUM
 Tarehe: 01/08/2014
SERIKALI kupitia Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni, na Michezo imewataka Makocha wa Mpira wa Miguu wanaopata mafunzo ya siku mbili kutoka kwa makocha wa Timu ya FC Bacelona waliotoka Spain kuinua mchezo wa Mpira wa miguu hivyo kuitangaza nchi ya Tanzania kimataifa.

Kauli hiyo imetolewa na Kaimu Mkurugenzi Maendeleo ya Michezo Bibi. Juliana Yassoda wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya Makocha 30 wa Mpira wa Miguu yaliyoandaliwa na Tanzania Brweweries Limited kupitia kinywaji cha Castle Lager leo jijini Dar es Salaam katika Uwanja wa Karume.

Bibi. Yassoda amesema kuwa Wizara inatamani kuona wachezaji, klabu pamoja na timu za taifa kuwa katika nyanja ya kimataifa kwani michezo ni shughuli za kiuchumi, kimichezo na kijamii haswa mpira wa miguu unaovutia duniani kote.

Akitoa wosia kwa makocha Bibi. Yassoda amewaomba washiriki kuwa makini na kuwa na nidhamu wakati wa mafunzo ili kuongeza ujuzi pia kuwa na uhakika na serikali yao kwani serikali itaendelea kujenga mazingira mazuri na wawekezaji kiuchumi na kijamii katika sekta ya michezo kwa manufaa ya watanzania wote.

Aidha Balozi wa Spain nchini Tanzania Bw. Luis Manuel Ceuesta Civis ameishukuru kampuni ya Tanzania Breweries kupitia bia yao ya Castle Lager kuandaa mafunzo hayo kwa makocha na kuwataka makocha wanaoshiriki mafunzo hayo kuchukua ujuzi na kanuni za mpira kutoka kwa makocha wa FC Bacelona.

Naye Mkurugenzi wa Masoko kutoka Tanzania Breweries Limited Bi. Kushillah Thomas amewataka makocha wa Mpira wa Miguu kutoka Tanzania kupokea mafunzo maalum kutoka kwa wataalam wanaoongoza moja ya timu zenye mafanikio zaidi duniani kwa kutumia ujuzi mpya watakaoupata kuinua vipaji vya wachezaji na kuwaendeleza wanamichezo kuwa wanamichezo wa kimataifa.

No comments:

Post a Comment