TANGAZO


Saturday, July 5, 2014

Wananchi wayachangamkia Maonesho ya Sabasaba jijini Dar es Salaam

 Wananchi wakilishangaa gari linalotumia gesi badala ya mafuta walipotembelea banda la Wizara ya Nishati na Madini katika Maonesho ya Biashara ya Kimataifa, viwanja vya Mwalimu Nyerere, Dar es Salaam.(Picha zote na Kassim Mbarouk-www.bayana.blogspot.com)
Wananchi wakilishangaa gari linalotumia gesi badala ya mafuta walipotembelea banda la Wizara ya Nishati na Madini katika Maonesho ya Biashara ya Kimataifa, viwanja vya Mwalimu Nyerere, Dar es Salaam.
  Ofisa Uhusiano na Mawasiliano wa Mfuko wa Pesheni (PPF), Lulu Mengele, akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kazi na majukumu ya mfuko huo kwa jamii kwenye banda la PPF
 Mtaalamu wa Ushirikishaji wadau wa Shirika la Changamoto za Milenia (MCC), Rehema Mbulalina, akiwapatia maelezo wadau waliotembelea banda hilo lililopo ndani ya Banda la Wizara ya Fedha, katika Maonesho ya Biashara ya Kimataifa yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Nyerere, jijini Dar es Salaam.
Mwanafunzi wa Veta, Rehema Omary akiwapatia maelezo wananchi waliotembelea banda la Veta kuhusu injini ya gari inavyofanya kazi, katika maonesho hayo. 

No comments:

Post a Comment