TANGAZO


Tuesday, June 3, 2014

Wapinga marufuku ya maandamano Nigeria






Waandamanji waliofika mahakamani kupinga marufuku ya maandamano Abuja

Watu wanaounga mkono maandamano ya kushinikiza serikali kuwanusuru wasichana zaidi ya miambili waliotekwa nyara na wanamgambo wa kiisilamu nchini Nigeria wamepinga hatua ya mahakama kupiga marufuku maandamano mjini Abuja.
Polisi wametaja maandamano hayo kama tisho kwa usalama wa nchi hiyo.


Kampeni hii imekuwa ikiendelea tangu wasichana kutekwa nyara Nigeria
Maandamano hayo yamekuwa yakifanyika kuishinikiza serikali kuongeza kasi juhudi zake za kuwanusuru wasichana hao waliotekwa nyara na Boko Haram zaidi ya mwezi mmoja uliopita.
Kauli mbiu ya maandamano hayo ni ''Bring Back Our Girls'' yaani turejesheeni watoto wetu, na waandamanaji wanasema kuwa maandamano yao yalikuwa ya amani.
Kundi la kiisilamu la Boko Haram, limesema kuwa liko tayari kuwaachilia wasichana hao ikiwa serikali nayo itawaachilia wapiganaji wake wanaozuiliwa.

No comments:

Post a Comment