TANGAZO


Tuesday, June 10, 2014

Kikao cha Kamati ya Ufundi ya TCD

 *Wajumbe wahoji ukweli wa UKAWA kulipwa sh. 450,000 kwa siku
 kwa kutohudhuria vikao vya Bunge hilo na Taasisi za Nje
 
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Philip Mangula akifafanua jambo mbele ya waandishi wa Habari alipowaita White House kuwaambia walichojadili Jumapili iliyopita na viongozi wa UKAWA kuhusu namna watakavyojenga maelewano katika Bunge la Katiba kilichoandaliwa na Technical Committee (TCD).
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Philip Mangula akifafanua jambo mbele ya waandishi wa Habari alipowaita White House kuwaambia walichojadili Jumapili iliyopita na viongozi wa UKAWA kuhusu namna watakavyojenga maelewano katika Bunge la Katiba kilichoandaliwa na Technical Committee (TCD).
Jengo la Makao Makuu ya Chama Cha Cha Mapinduzi (CCM), lililopo katikati ya Barabara ya Tano na ya Sita Mijini Dodoma. (Picha zote na John Banda)
Jengo la Makao Makuu ya Chama Cha Cha Mapinduzi (CCM), lililopo katikati ya Barabara ya Tano na ya Sita Mijini Dodoma.
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Philip Mangula akifafanua jambo kwa waandishi wa Habari alipowaita White House kuwaambia walichojadili Jumapili iliyopita na viongozi wa UKAWA.

Na Joyce Kasiki, Dododoma
WAJUMBE  wa Bunge la Katiba wanaounda Umoja wa Katiba ya wananchi (UKAWA), ambao hawatahudhuria vikao vya bunge hilo, watalipwa sh. 450,000 na taasisi za Ujerumani, zinazofadhili umoja huo, imeelezwa.

Mwenyekiti wa kikao cha Kamati ya Ufundi  ya TCD, Philip Mangula alisema suala hilo, lilibuka katika kikao  cha Kamati ya Ufundi ya TCD ambacho kilikutana leo, ili kujadili na kupata sababu ya wanachama wa UKAWA kususia Bunge la Katiba.
 
"Katika kikao chetu ambacho tulikutana Juni 8, 2014, pamoja na mambo mengine wajumbe pia walitaka kusikia kauli ya UKAWA kuhusu tuhuma nzito zilizotolewa kwenye vyombo vya habari, kwamba kumefanyika uchunguzi na vyombo hivyo uliobaini kuwa, yapo mashirika mawili yanayowafadhili washiriki wa UKAWA kwa kutohudhuria vikao vya Bunge maalum.

"Mashirika yaliyotajwa kuwafadhili UKAWA wasihudhurie Bunge hilo ni Chama cha CDU cha Ujerumani na Chama cha Conservative cha Uingereza. 
 
Aidha taarifa hizo zinaeleza kuwa taasisi ya Democratic Union Of Africa (DU-Africa), inafadhili UKAWA.

"Taarifa  hizo zinaonesha kuwa kuwa, mwezi Machi mwaka huu UKAWA ilipokea sh.bilioni 1.7 na baadaye ilipokea sh.380 milioni huku kuliwa na ahadi ya kupatiwa kiasi kingine cha sh.bilioni 3.2 Baada ya kupeleka marejesho ya matumizi ya mgawo wa kwanza." alisema Mangula.

Hata hivyo alisema  wahusika wakuu waliotakiwa kutoa ufafanuzi juu ya jambo hilo hawakuhudhuria kikao hicho ,wajumbe wa Baraza wa kikao hicho wamekubaliana kuitisha kikao cha Baraza la Taifa la vyama vya Siasa linalojmuisha vyama vyote 22 vyenye usajili wa kudumu ili kuendelea kutafakari hatma ya mchakato wa katiba wa awamu ya pili unaotarajiwa kuanza mwezi August mwaka huu. 

 Aidha Mangula aliwaambia waandishi kuwa lengo la kikao hicho lilikuwa ni kujadiliana kwa pamoja na kujua sababu zilizowafanya baadhi ya wajumbe waliuounda UKAWA ambao haumo katika mchakato wa  uundaji wa katiba.

Alisema hata hivyo wajumbe walishindwa kufikia azma yao kutokana na kutokuwepo kwa wawakilishi wa vyama hivyo ili kupata maelezo fasaha ya kiini cha tatizo lililowasukuma kususia Bunge la katiba licha ya kwamba ndani ya kanuni za Bunge hilo kuna utaratibu uliowekwa wa kutatua matatizo na kutoelewana kunakotokea ndani ya Bunge hilo.

"Bunge limeweka Kamati ya maridhiano na pia Kamati ya uongozi ambazo hujadili matatizo yatokeapo baina yao au  miongoni mwa wabunge hao." alisema Mangula

Kamati hiyo ya Ufundi ina wawakilishi kutoka vyama vyote vinavyounda TCD ambavyo ni CCM, Chadema, CUF, NCCR-Mageuzi, TLP na UDP huku cha UPDP kikiwakilisha vyama visivyo na wabunge.

No comments:

Post a Comment