TANGAZO


Wednesday, April 2, 2014

Mkuu wa polisi auawa nchini Misri


Mashambulizi dhidi ya polisi Misri yamekuwa yakiongezeka
Brigedia Jenerali wa jeshi la polisi nchini Misri ameuawa katika milipuko miwili tofauti iliyotokea kwa wakati mmoja karibu na chuo kikuu cha Cairo.
Vyombo vya habari vinasema kuwa watu wengine wanne walijeruhiwa katika mashambulizi hayo.
Kwa mujibu wa maafisa wa usalama, mabomu yalikuwa yametegwa karibu na kituo cha polisi.
Hauna kundi lolote limekiri kufanya mashambulizi hayo.
Misri imekuwa ikikumbwa na mashambulizi ya mara kwa mara dhidi ya taasisi za serikali yanayofanywa na makundi ya wapiganaji hasa baada ya kupinduliwa kwa aliyekuwa Rais Mohammed Morsi mwezi Julai.

No comments:

Post a Comment