Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akihutubia wakati akizindua rasmi Kongamano la 28 la Mwaka la Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Tiba (NIMR). Kongamano hilo lililofanyika kwenye Ukumbi wa Mwalimu Nyerere, jijini Dar es Salaam, limeandaliwa na Taasisi hiyo ya (NIMR).
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akikata utepe kuashiri kuzindua Mpango wa Mkakati wa Nne wa Utafiti Bora wa Afya, wakati wa ufunguzi wa Kongamano la 28 la Mwaka la Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Tiba (NIMR), lililofanyika kwenye Ukumbi wa Mwalimu Nyerere, jijini Dar es Salaam. Kongamano hilo limeandaliwa na Taasisi hiyo ya (NIMR). Kushoto ni Mkurugenzi wa NIMR, Dkt. Mwele Malecela (katikati) ni Mwenyekiti wa Baraza la NIMR, Samwel Masele.
Picha ya pamoja na washiriki wa Kongamano hilo. (FS)

No comments:
Post a Comment