TANGAZO


Saturday, July 13, 2013

Mkuu wa Mkoa Morogoro, Joel Bendera aufungua mkutano maalum wa TFF jijini Dar es Salaam


Mkuu wa Mkoa Morogoro, ambaye alikuwa mgeni rasmi wa mkutano huo, Joel Bendera (kushoto) akiwa na Mwakilishi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani (FIFA), James Johnson (katikati) pamoja na Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodegar Tenga wakati wa Mkutano Mkuu maalum wa TFF, kwenye Ukumbi wa NSSF WaterFront,Dar es Salaam.
Johnson wa FIFA akimpongeza Rais wa TFF, Leodegar Tenga baada ya kuhutubia
Sehemu ya wajumbe wakiwa kwenye Mkutano Mkuu maalumu wa TFF, Dar es Salaam jana. Mstari wa mbele kutoka kushoto ni wajumbe wa Mkoa wa Dar es Salaam, Msanifu Kondo, Benny Kisaka na Almasi Kasongo na Dunstaun Mkundi kutoka Mkoa wa Lindi.
 Viongozi wakiomba dua wakati wa ufunguzi wa mkutano huo. Kutoka kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Morogoro ambaye alikuwa mgeni rasmi katika mkutano huo, Joel Bendera, Mwenyekiti wa Baraza la Michezo la Taifa(BMT), Dioniz Malinzi, Makamu wa Kwanza wa Rais wa TFF, Athuman Nyamlani na Makamu wa Pili wa Rais wa TFF, Ramadhan Nasibu.
Wajumbe wakiomba dua kabla ya kuanza  mkutano huo. Kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa Kagera Sugar, Yahya, Mwenyekiti wa Klabu ya Azam FC, Said Mohamed na Ahmed Aurora ambaye ni mwenyekiti wa Coastal Union
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodeger Tenga akihutubia mkutano huo.
 Mwakilishi wa FIFA, Johnson akitoa maneno yake kwenye kutano huo
 Mwenyekiti wa BMT, Malinzi akihutubia katika mkutano huo
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro ambaye alikuwa mgeni rasmi katika mkutano huo, Joel Bendera, akihutubia wakati wa ufunguzi wa Mkutano Mkuu maalum wa TFF, kwenye Ukumbi wa NSSF WaterFront, Dar es Salaam leo.
Mwanahabari wa gazeti la Jambo Leo, Asha Kigundula, akiwa kazini kwenye mkutano huo leo.

No comments:

Post a Comment