TANGAZO


Friday, February 8, 2013

Makamu wa Rais, Dk. Bilal alipokutana na Seneta Steve King, Viongozi wa Jumiya ya Watanzania waishio Washington DC, nchini Marekani kwa mazungumzo


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Seneta, Stive King, wakati alipofika katika Ofisi yake iliyopo katika jengo la Ofisi za Maseneta wa Marekani, akiwa katika ziara yake ya siku nne katika jiji la Washington Dc, nchini Marekani, juzi Feb 6, 2013.

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na baadhi ya viongozi wa Jumuiya ya Watanzania waishio Washington Dc juzi, Feb 6, 2013.

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na baadhi ya viongozi wa Jumuiya ya Watanzania waishio Washington Dc, baada ya mazungumzo yao yaliyofanyika juzi, Feb 6, 2013, Hoteli ya Omni Shoreham.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Ubalozi wa Tanzania, nchini Marekani katika jiji la Washington Dc, baada ya mazungumzo yao alipowasili jijini humo kuanza ziara yake ya siku nne, iliyomalizika jana Feb 7, 2013. Wa kwanza kushoto ni Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu, wa tano kushoto ni Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mahadhi Juma Maalim. (Picha zote na Muhidin Sufiani-OMR) 

No comments:

Post a Comment