TANGAZO


Friday, February 8, 2013

Maofisa Habari wa Serikali watembelea Kikao cha Bunge, Mjini Dodoma

Baadhi ya Maofisa Habari na Mawasiliano Serikalini,  wakielekea katika ukumbi wa mkutano wa Bunge jana, mjini Dodoma. Maofisa hao, wamefanya ziara  bungeni hapo, ili kuona  shughuli mbalimbali za Bunge. 

Baadhi ya Maofisa Habari na Mawasiliano Serikalini, wakiongozwa na Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO), Assah Mwambene (wanne kushoto, mstari wa mbele), wakiwa ndani ya ukumbi wa Bunge jana kuangalia shughuli mbalimbali za Bunge, mjini Dodoma.

Baadhi ya Maofisa Habari na Mawasiliano Serikalini, wakiwa ndani ya ukumbi wa Bunge, mjini Dodoma jana, wakifuatilia jinsi Bunge hilo linavyoendeshwa.

Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Aggrey Mwanri akiwakilisha hati mezani kuhusu Taarifa ya Mwaka na Hesabu zilizokaguliwa na Mfuko wa Pensheni wa Serikali za Mitaa kwa Mwaka wa Fedha, 2010/2011.

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Pereira Silima, akiwasilisha Azimio la Bunge la Kujiunga na Mkataba wa Kimataifa wa Kuzuia Vitendo vya Ugaidi wa Kutumia Nyuklia. Azimio hilo limeungwa mkono jana  katika  mkutano wa kumi, kikao cha nane.

Waziri wa  Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Shukuru Kawambwa (kulia), akiongea  na Wabunge, James Mbatia (kushoto) na Charles Mwijage (Muleba Kaskazini), katika viwanja vya Bunge, mjini Dodoma jana, baada ya Spika Anne Makinda (hayupo pichani), kutangaza rasmi kwamba Mitala ya  Elimu inayotumika ni halali na ipo. 

Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji  Frederick Werema akisoma Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria mbalimbali wa mwaka 2012 katika ukumbi wa Bunge leo.


Mwenyekiti wa Bunge, Mussa Azzan 'Zungu', akizungumza wakati akikiendesha kikao hicho cha Bunge jana.



Mwenyekiti wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe (kushoto) na Mbunge Joshua Nassari, wakitetea jambo wakati wa kikao hicho cha Bunge jana. (Picha zote na Mwanakombo Jumaa-MAELEZO)

No comments:

Post a Comment