TANGAZO


Tuesday, January 1, 2013

Viongozi wa M23 wawekewa vikwazo na UM

 

Mpiganaji wa M23 akiwa na chombo cha mawasiliano
 
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, limewawekea vikwazo viongozi wa kundi la waasi wa M23 nchini Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
 
Chini ya sheria hiyo, mali ya watu watakaohusishwa na kundi hilo itapigwa tanji na kuzuiliwa kusafiri katika mataifa ya nje.
Kundi hilo la M23 lililoundwa na wanajeshi waasi,waliuteka mji wa Goma, Mashariki mwa Congo karibu na mpaka wa nchi hiyo na Rwanda, kutoka kwa wanajeshi wa serikali na wale wa kutunza amani wa Umoja wa Mataifa.

Waasi wa M23 washurutishwa kuondoka Goma

Lakini kufuatia shutuma kutoka kwa jamii ya kimataifa wapiganaji hao walikubali kuondoka kutoka mjini humo mwezi uliopita.

Tangazo hilo limetolewa mkesha wa siku ya mwaka mpya siku moja tu kabla ya Rwanda kujiunga kuwa mwanachama wa baraza hilo la Usalama la Umoja wa Mataifa kwa kipindi cha miaka miwili.

Umoja wa Mataifa na Serikali ya Congo, zimeishutumu serikali za Rwanda na Uganda kwa kuwaunga mkono wapiganaji hao wa waasi, madai ambayo yamepingwa vikali za serikali hizo mbili.

Rwanda inatuhumiwa kuunga mkono makundi ya waasi Mashariki mwa Congo, kama njia moja ya kupambana na wapiganaji wa waasi wa Kihutu ambao walitoroka nchini humo baada ya mauaji ya kimbari miaka ya tisini

No comments:

Post a Comment