TANGAZO


Saturday, January 12, 2013

Makamu wa Rais, Dk. Gharib Bilal ahudhuria Sherehe za miaka 49 ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mjini Unguja


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,
Dk. Ali Mohamed Shein, akikagua Gwaride wakati wa Sherehe za Mapinduzi, zilizofanyika leo kwenye Uwanja wa Amani mjini Zanzibar.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na Rais mstaafu wa Zanzibar, Dk. Salmin Amour, wakati alipowasili Uwanja wa Amani, Mjini Zanzibar leo, kwa ajili ya kuhudhuria sherehe za Mapinduzi ya Zanzibar. 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad, wakati alipowasili kwenye Uwanja wa Amani, Mjini Zanzibar leo, kwa ajili ya kuhudhuria katika sherehe za Mapinduzi ya Zanzibar.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Pandu Ameir Kificho, wakati alipowasili kwenye Uwanja wa Amani, Mjini Zanzibar leo kwa ajili ya kuhudhuria katika sherehe za Mapinduzi ya Zanzibar.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
 
Dk. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na Waziri Mkuu
 
mstaafu, Edward Lowassa, wakati alipowasili Uwanja
 
wa Amani Mjini Zanzibar leo kwa ajili ya kuhudhuria katika
 
sherehe za Mapinduzi ya Zanzibar.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Mohammed Gharib Bilal (kushoto), akiteta na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad, wakati wa maadhimisho ya miaka 49 ya Mapinduzi ya Zanzibar.


Mke wa Rais Mstaafu, Mama Siti Mwinyi, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Shamsi Vuai  Nahodha, Mke wa Makamu wa Rais, Mama Asha Bilal na Waziri Mkuu mstaafu, Fredrick Sumaye, wakiwa kwenye maadhimisho ya miaka 49 ya Mapinduzi ya Zanzibar, Uwanja wa Aman, mjini Unguja leo.

Kikosi cha Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), kikipita kwa mwendo wa pole, mbele ya Rais wa Zanzibar, Dk. Shein wakati wa maadhimisho hayo, uwanjani hapo leo. (Picha zote na OMR)

No comments:

Post a Comment