TANGAZO


Saturday, January 12, 2013

Abiria wa Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL), wanusurika kufa

 
Na Magreth Magosso,Kigoma
ZAIDI ya abiria 25 wamenusurika kufa, baada ya ndege  waliyokuwa wakisafiria ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL), kutoka Kigoma kuelekea Dar es Salaam  kupata hitilafu ikiwa angani, jambo lililomlazimu rubani wa ndege hiyo kuirudisha tena mkoani Kigoma.
 
Hali hiyo, imetokana jana  saa kumi jioni, ambapo moja ya vioo vya mbele ya ndege hiyo kilipasuaka na hivyo kuruhusu upepo mkali kuingia ndani na kuwafanya marubani wa ndege hiyo, kufanya kazi ya ziada kuhakikisha ndege, inatua salama katika Kiwanja cha ndege Kigoma.
Ndege hiyo  ilikuwa katika safari yake ya kwanza kwa mwaka huu, mkoani humo, ikiwa ni zaidi ya miezi 10 baada ya ndege nyingine ya shirika hilo, kuanguka na mabaki yake kutelekezwa katika kiwanja cha ndege kigoma huku sintofahamu ya kuondolewa kwa mabaki hayo.
Wakiongea kwa nyakati tofauti baadhi ya abiria waliokuwemo kwenye ndege hiyo Athumani Batumwa na Fred Mbassa walisema ndege hiyo inauwezo wa kubeba abiria 50 ambapo ilipata itilafu baada ya dakika 30 kuanza kuruka kwa chombo hicho kutoka kwenye uwanja wa ndege kigoma.
Kaimu meneja wa shirila la ATCL, Kepten Milton Lazaro amekiri kutokea kwa itilafu hiyo na amewaondoa hofu wadau wa usafiri huo, juu ta tatizo hilo na kwamba ni sehemu ya matatizo yanayoweza kutokea kwa ndege yoyote.
Alisema kuwa utaratibu unafanywa kuhakikisha kwamba abiria waliokuwa wakisafiri na ndege hiyo wanatafutiwa ndege nyingine na kwamba hadi kufikia leo abiria hao watakuwa wameshatafutiwa ufumbuzi lakini pia ndege hiyo inaweza kuanza kufanyiwa marekebisho kuanzia baada ya kuwasili kwa spea.

No comments:

Post a Comment