TANGAZO


Saturday, November 24, 2012

Ziara ya Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahaman Kinana Arusha


Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahman Kinana akisalimiana na Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowassa kwenye Uwanja wa Ndege wa Arusha leo. Kushoto ni Katibu wa CCM Mkoa wa Arusha, Mary Chatanda.

Pikipiki zikiongoza msafara wa Kinana, kutoka Uwanja wa Ndege wa Arusha kuelekea mjini.

Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahaman Kinana akipandisha bendera ya chama hicho, kuashiria ufunguzi wa Shina la Wakereketwa Wajasiriamali wa CCM, Nguruma, Arumeru, Arusha.

Wananchi wa kabila la Kimasai, wakicheza ngoma, wakati wa mkutano wa CCM, Meru, Arusha.

Katibu Mkuu wa CCM, Kinana akisalimia wananchi baada ya kuwasili Viwanja vya Usa River, kuhutubia mkutano wa hadhara.

 Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowassa (kulia), akiteta jambo na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye katika mkutano uliohutubiwa na katibu Mkuu, Abdulrahman Kinana.

Baadhi ya vijana 150 wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), waliohamia CCM, wakionesha kadi zao za zamani wakiwa Chadema, wakati wa mkutano wa Usa River.

Wazee wa Kimeru, wakimkabidhi vitendea kazi vya jadi, Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahaman Kinana katika mkutano wa hadhara uliofanyika Usa River, Arusha. Anayemkabidhi ni Ezrom Sumari.

Katibu Mkuu Kinana akivishwa mavazi ya jadi ya Wameru, wakati wa mkutano uliofanyika Usa River, Arusha leo.

Kinana akiwa na zana za jadi alizokabidhiwa kwa heshima yake na wazee wa Kimeru katika Mkutano wa CCM uliofanyika Usa River, Arusha. (Picha zote na mpigapicha wetu)

No comments:

Post a Comment