
Mwandishi wa BBC mjini humo anasema kumetokea miripuko miwili mikubwa nje ya mkahawa huo uitwao "The Village", katika mtaa wa Hodan, kati-kati ya mji.
Walioshuhudia tukio hilo wanasema mabomu yaliripuliwa na watu waliojitolea mhanga.
Mwezi wa Septemba watu 14 walikufa kwenye shambulio katika mkahawa mwengine mjini Mogadishu wa tajiri huyo-huyo.
Mwandishi wa BBC anakumbusha kuwa mashambulio kama hayo hufanywa mara kwa mara, na baadhi yao ni vitendo vya kundi la wapiganaji wa Kiislamu, al-Shabaab, ambao bado wanadhibiti sehemu kubwa ya nchi.
Mashambulio mengine hufanywa na magengi ya wahalifu na wanamgambo.

No comments:
Post a Comment