Mabingwa wa Mashindano ya
Mitumbwi ya Balimi Mkoa wa Mwanza, timu ya Cheka na Wengi kutoka Misungwi,
wakiwasili ufukweni baada ya kuongoza mbio hizo, zilizofanyika Mwaloni mkoani
humo juzi.
Nahodha wa timu iliyoshinda ya wanaume kutoka Misungwi, Daniel Mugeng'a, akionesha kitita cha shilingi laki tisa baada ya kukabidhiwa juzi.
Mabingwa
wa mashindano ya Mitumbwi ya Balimi (Balimi Boat Race), mkoani Mwanza upande wa
wanawake, timu ya Wanawake na Maendeleo kutoka Misungwi, wakiwa hawaamini macho yao kama
wameweza kushinda kwa kuwaacha mbali wenzao na kuwa mabingwa wa mkoa huo na
kukabidhiwa jumla ya shilingi laki saba (700,000), kama zawadi ya ushindi wa
kwanza.
Wapiga makasia
wakinyanyua makasia yao juu kabla ya kuanza kwa fainali za mashindano ya
mitumbwi ya Balimi (Balimi Boat Race), yaliyofanyika jijini Mwanza juzi.
| Baadhi ya wapiga makasia wakinyanyua makasia yao juu kabla ya kuanza kwa fainali za mashindano ya mitumbwi ya Balimi (Balimi Boat Race), yaliyofanyika jijini Mwanza juzi. |
Mabingwa
wa ngoma za asili wa mashindano ya ngoma ya Kanda ya Ziwa, kikundi cha Bujora
wakitumbuiza mashabiki wa mashindano ya mitumbwi, yaliyofanyika kwenye fukwe za
Mwaloni mkoani Mwanza, ambapo washindi watakaowakilisha mkoa huo, kwenye fainali
wamepatikana.
Meneja
Masoko wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Fimbo Butala (kushoto), akiteta jambo na Afisa Utamaduni na
Michezo wa Manispaa ya Ilemela, wakati wa mashindano ya Mitumbwi ya Balimi
(Balimi Boat Race), yaliyofanyika mkoani Mwanza juzi.
Msanii
wa kikundi cha ngoma cha Bujora, akicheza na nyoka kwa kuingiza kichwa chake mdomoni
wakati kikitumbuiza wananchi waliofika kushuhudia mashindano ya mitumbwi ya Balimi
(Balimi Boat Race), yaliyofanyika Mwaloni mkoani Mwanza juzi.
Meneja
Masoko wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Fimbo Butallah, akimuelekeza jambo Nahodha
wa timu ya Wanawake na Maendeleo ya Misungwi, Tabu Daudi, ambao ndio washindi wa
kwanza kwa upande wa wanawake Mkoa wa Mwanza mara baada ya kukabidhiwa zawadi
yao ya ushindi wa kwanza kitita cha shilingi laki saba (700,000).
| Baadhi ya wananchi waliohudhuria mashindano hayo, wakifuatilia matukio mbalimbali yaliyokuwa yakitendeka katika mashindano hayo. (Na Mpiga Picha Wetu) |

No comments:
Post a Comment