TANGAZO


Monday, October 29, 2012

Serikali ya Zanzibar yakabidhi ubani kwa familia ya marehemu Koplo Said Abdulrahman mjini Zanzibar leo

Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja, Abdalla Mwinyi Khamis (katikati), akitoa nasaha zake kwa wanafamilia wa marehemu Koplo Said Abdulrahman Juma wa Jeshi la Polisi, alipofika kukabidhi fedha kwa ajili ya ubani kwa niaba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein, nyumbani kwa wafiwa, Nyerere mjini Zanzibar leo. Wengine kutoka kushoto ni Mkuu wa Jeshi la  Polisi Tanzania, IGP Said Ali Mwema, kulia ni Kamishna wa Polisi Zanzibar, Mussa Ali Mussa na Afisa Tawala Mkoa wa Mjini Magharibi, Ayoub Mohamed Mahamoud. Hafla hiyo ilifanyika leo. (Picha zote na Ramadhan Othman, Ikulu)

Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja, Abdalla Mwinyi Khamis (kulia), akikabidhi fedha kwa ajili ya ubani kwa niaba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein, nyumbani kwa wafiwa wa marehemu Koplo Said Abdulrahman Juma wa Jeshi la Polisi, Nyerere mjini Zanzibar leo kwa niaba ya wanafamilia wa marehemu. Baba Mdogo Juma Omar Salum (wa pili kushoto), akipokea ubani huo. Wa pili kulia ni Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania, IGP Said Mwema na kushoto ni Baba mzazi wa marehemu, Abdulrahman Juma Hassan.

Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja, Abdalla Mwinyi Khamis (kulia), akiagana na baba wa marehemu Koplo Said Abdulrahman Juma wa Jeshi la Polisi, mara baada ya kukabidhi ubani kwa wafiwa kwa niaba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein, nyumbani kwa wafiwa, Nyerere mjini Zanzibar leo. 

No comments:

Post a Comment