TANGAZO


Tuesday, July 10, 2012

Rais wa Chama cha Madaktari afikishwa Mahakama ya Kisutu



 Jengo la Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, alipopelekwa Rais wa Chama cha Madaktari Tanzania (MAT), Namala Mkopi leo, kusomewa shitaka la kutokutii amri halali ya Mahakama Kuu, iliyomtaka kuwatangazia wanachama wa chama hicho kupitia vyombo vya habari, kusitisha mgomo wao.
 Rais wa Chama cha Madaktari Tanzania (MAT), Dk. Namala Mkopi akiwa chini ya ulinzi wa askari Polisi na Magereza, wakati akiingia Mahakamani Kisutu leo kwa ajili ya kusomewa shitaka hilo.
 Rais wa Chama cha Madaktari Tanzania (MAT), Dk. Namala Mkopi akiwa chini ya ulinzi wa askari Polisi wakati akiingia Mahakamani leo.
  Rais wa Chama cha Madaktari Tanzania (MAT), Dk. Namala Mkopi akiwa chini ya ulinzi wa askari Polisi wakati  akisindikizwa kuingia Mahakama ya Kisutu kwa kusomewa shitaka linalomkabili la kutotii amri halali ya Mahakama Kuu iliyomtaka kuwatangazia wanachama wa chama hicho kupitia vyombo vya habari, kusitisha mgomo wao.
 Rais wa Chama cha Madaktari Tanzania (MAT), Dk. Namala Mkopi akiwa na mama yake mzazi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam leo mara baada ya kusomewa shitaka lake hilo. 
 Rais wa Chama cha Madaktari Tanzania (MAT), Dk. Namala Mkopi (kulia) akiongozana na baba yake mdogo, Hilary Chinendachi mara baada ya kupoata dhama katika Mahakama ya Hakimu Makazi Kisutu jijini Dar es Salaam leo, aliposomewa shiataka lake hilo.
 Rais wa Chama cha Madaktari Tanzania (MAT), Dk. Namala Mkopi akipeana mikono na baadhi ya madaktari waliofika kujua hatma yake baada ya kufikishwa Mahakamani kwa kosa la kukaidi amri ya Mahakama Kuu iliyomtaka kuwatangazia wanachama wa chama hicho, kupitia vyombo vya habari kusitisha mgomo wao.
Rais wa Chama cha Madaktari Tanzania (MAT), Dk. Namala Mkopi akiwa na mama yake mzazi (katikati), pamoja na baba yake mdogo, Hilary Chinendachi mara baada ya kupatiwa dhama katika Mahakama ya Hakimu Makazi Kisutu jijini Dar es Salaam leo.
Rais wa Chama cha Madaktari Tanzania (MAT), Dk. Namala Mkopi, akizungumza jambo na Mwanasheria ambaye pia ni wakili wake, Kikondo Maulidi (kushoto), baada ya kuachiwa kwa dhamana, Mahakama ya Kisutu leo. (Picha zote na Kassim Mbarouk, Francis Dande)

No comments:

Post a Comment