TANGAZO


Friday, May 18, 2012

Ndege mpya ATC yaanza safari zake

Kaimu Mkurugenzi wa Shirika la ndege la ATC, Paul Chizii (kulia), akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa kampuni hiyo, mara baada ya ndege mpya ya Shirika hilo kutua katika Uwanja wa ndege wa Mwanza mchana huu ambapo wafanyakazi pamoja na watu mbalimbali ambao wamekuwa wakitumia ndege za shirika hilo katika kusafiri wameonekana kufurahia sana kuanza kwa safari za shirika hilo. Katika Uwanja wa ndege wa Mwanza kutakuwa na hafla fupi ya kupongezana kwa ajili ya kuikaribisha ndege hiyo ambapo pia keki itakatwa kwa ajili ya uzinduzi rasmi wa safari zake.
 
Abiria mbalimbali wakishuka mara baada ya ndege hiyo kuwasili jijini Mwanza mchana wa leo.
 
Dada Lilian wa ATC, akiwa katika pozi mara baada ya kushuka kwenye ndege hiyo leo jijini  Mwanza.
 
Abiria wakishuka kwenye ndege hiyo mpya ya Shirika la Ndege Tanzania (ATC).
 
Abiria wakishuka kwenye ndege jijini Mwanza, wakati ndege mpya ya Shirika la ndege Tanzania (ATC), ilipowasili ikiwa ni safari yake ya mwanzo tokea iwasili nchini mwanzoni mwa wiki. (Picha zote na John Bukuku wa Fullshangwe)

No comments:

Post a Comment